Saturday 24 January 2009

Mabingwa Watetezi Kombe la FA Portsmouth watolewa na Timu ya Daraja la Chini Swansea!!
Aston Villa watoka suluhu na Timu ndogo Doncaster!!!


Mabingwa Watetezi wa FA Cup, Portsmouth, wamekula kipigo mbele ya umati wa Mashabiki wake nyumbani cha mabao 2-0 na Swansea ambao wako Daraja la chini ya LIGI KUU na kuaga mashindano hayo ya Kombe la FA.
Magoli ya kipindi cha kwanza yaliyofungwa na Nathon Dyer dakika ya 26 na Jason Scotland dakika ya 45 kwa penalti ndio yaliyowaua Portsmouth.
Nao Aston Villa, wakicheza ugenini nyumbani kwa Doncaster, timu iliyo Daraja la Chini, ilibanwa na kutoka suluhu na sasa mechi itarudiwa nyumbani kwa Aston Villa.
Lakini kwenye dakika ya 87 Aston Villa walinusurika kufungwa baada ya frikiki ya Woods kumshinda Kipa Brad Friedel na kugonga besera.

MATOKEO KAMILI RAUNDI YA 4 KOMBE LA FA:

Hartlepool 0-2 West Ham
Chelsea 3-1 Ipswich
Doncaster 0-0 Aston Villa
Hull City 2-0 Millwall
Kettering 2-4 Fulham
Portsmouth 0-2 Swansea
Sheff United 2-1 Charlton
Sunderland 0-0 Blackburn
Torquay 0-1 Coventry
Watford 4-3 Crystal Palace
West Brom 2-2 Burnley
Wolves 1-2 Middlesbrough

Mechi inayofuata saa 2 na robo usiku: Manchester United v Tottenham

No comments:

Powered By Blogger