Sunday 18 January 2009

Tottenham 1 Portsmouth 1

Hii ni mechi iliyowafanya Meneja wa Tottenham Harry Redknapp na Mchezaji wake Jermaine Defoe kupambana na Klabu yao ya zamani kwa mara ya kwanza tangu waihame muda si mrefu uliopita.
Na alikuwa Defoe alieiokoa Tottenham kufungwa pale aliposawazisha kwa bao la dakika ya 70.
Portsmouth walifunga bao lao dakika ya 59 kupitia David Nugent kwenye dakika ya 59.

MECHI LIGI KUU: LIVERPOOL v EVERTON

LEO JUMATATU 19 JANUARI 2009 SAA 5 USIKU [saa za bongo]

Leo usiku Uwanjani Anfield, Liverpool watawakaribisha jirani zao wakazi wa mji mmoja, mji wa Liverpool, Timu ya Everton ambao ni wapinzani wao wa jadi.
Liverpool, waliocheza mechi 21 za LIGI KUU na wana pointi 46 pointi moja nyuma ya vinara wa ligi hiyo Mabingwa Manchester United waliocheza mechi 21 na kuwa na pointi 47, wanahitaji ushindi ili wachukue tena uongozi wa ligi hiyo baada ya kupitwa na Man U siku ya Jumamosi.
Nao Everton wako nafasi ya 7 na wana pointi 35.
Liverpool watawakaribisha kikosini Xabi Alonso na Fernando Torres ambao wote walikuwa majeruhi na sasa wamepona.
Everton watamkosa Kiungo Marouane Fellaini ambae amefungiwa kwa kuwa na Kadi pamoja na majeruhi wa muda mrefu James Vaughan, Aiyegbeni Yakubu, Louis Saha, Nuno na Joseph Yobo.

TIMU ZITATOKANA NA:

Liverpool: Reina, Carragher, Arbeloa, Agger, Hyypia, Skrtel, Aurelio, Alonso, Benayoun, Lucas, Mascherano, Gerrard, Babel, Keane, Kuyt, Torres, Riera, Ngog, El Zhar, Cavalieri.

Everton: Howard, Hibbert, Baines, Jagielka, Lescott, Neville, Arteta, Pienaar, Castillo, Cahill, Anichebe, Nash, Van der Meyde, Rodwell, Gosling, Jutkiewicz, Kissock.

NUSU FAINALI CARLING CUP: Mechi za marudiano

20 Januari 2009 [saa 5 usiku bongo taimu] Manchester United v Derby County

Mechi ya kwanza Derby 1 Manchester United 0

21 Januari 2009 [saa 4 dak 45 usiku bongo taimu] Burnley v Tottenham

Mechi ya kwanza Tottenham 4 Burnley 1

Fainali itachezwa Wembley Stadium tarehe 1 Machi 2009.

No comments:

Powered By Blogger