Tuesday 10 February 2009

Edwin Van der Sar na Ngome yake: Dakika 1212 haijafungwa!!! Ni REKODI!!

Nae Ryan Giggs aweka rekodi: NI MCHEZAJI PEKEE ALIEFUNGA GOLI KILA MSIMU WA LIGI KUU TANGU IANZISHWE MIAKA 17 ILIYOPITA!!!

Kipa Edwin Van der Sar na Beki Nemanja Vidic ndio Wachezaji pekee waliocheza mechi zote 13 zilizoweka rekodi mpya, zenye jumla ya Masaa 20 na dakika 12 ikiwa ni sawa na dakika 1212, bila ya kufungwa hata goli moja kwenye mechi za LIGI KUU England.
Mara ya mwisho Man U kufungwa goli ilikuwa ni Novemba 8 mwaka jana wakati Sami Nasri alipoifungia Arsenal huko Emirates Stadium kwenye ushindi wao wa 2-1.
Mwezi uliokwisha, wakicheza na West Bromwich, Man U waliweka rekodi mpya ya LIGI za England ya kutofungwa muda mrefu.
Jumapili walipocheza na West Ham wameipita rekodi iliyowekwa na Aberdeen ya Scotland na kuwa Klabu ya kwanza Uingereza yote kutokufungwa goli kwenye LIGI za Uingereza [Uinigereza ikimaanisha Visiwa vya Uingereza yaani Scotland, Wales, Ireland pamoja na England].
Rekodi hiyo ya Aberdeen huku Kipa akiwa Bobby Clark iliwekwa kwenye Ligi ya Scotland msimu wa mwaka 1970/71 mwaka aliozaliwa Van der Sar!!!
Endapo Manchester United wataweza kuwazuia Fulham kufunga bao kwa Dakika 64 ya mechi yao ya kiporo ya LIGI KUU itakayochezwa Old Traford nyumbani kwa Mabingwa hao Jumatano ijayo tarehe 18 Februari, basi Manchester United wataivunja rekodi ya dunia inayoshikiliwa na aliekuwa Kipa wa Atletico Madrid Abel Renso ya kutokufungwa kwa Dakika 1275 katika mechi za Ligi.
RYAN GIGGS na rekodi yake!!!
Wakati Edwin Van der Sar anaweka rekodi akisaidiwa na Ngome yake ya Man U ikiongozwa na Nemanja Vidic kwenye mechi hiyo ya Jumapili waliyoishinda West Ham bao 1-0 goli lililofungwa na Ryan Giggs, nae Ryan Giggs kwa bao hilo aliweka rekodi mpya kwenye LIGI KUU England ya kuwa Mchezaji pekee alieweza kufunga goli kila msimu wa LIGI KUU hiyo tangu ianzishwe miaka 17 iliyopita.
LIGI KUU England ilianza rasmi tarehe 15 Agosti 1992.
Ryan Giggs alianza kuichezea Man U tangu Timu za Watoto lakini alianza kucheza Timu ya Kwanza rasmi tarehe 2 Machi 1991 akiwa na miaka 17 tu alipoingizwa kwenye mechi kumbadilisha Veterani Dennis Irwin Man U walipocheza na Everton.
Ryan Giggs kwa kucheza mechi hiyo ya juzi na West Ham amefikisha mechi 787 kwa Manchester United akiwa ni Mchezaji anaeongoza kwa kucheza mechi nyingi Manchester United.

No comments:

Powered By Blogger