Sunday 8 February 2009

Beckham yumo Kikosi cha England kupambana na Spain Jumatano

Meneja wa England Fabio Capello amemwita kikosini David Beckham ambae kwa sasa yuko kwa mkopo AC Milan kutoka Klabu yake ya Marekani LA Galaxy na endapo atacheza mechi ya kirafiki na Spain hapo Jumatano huko Spain atakuwa amefungana na Bobby Moore kwa kuchezea mechi 108 Timu ya Taifa ya England ikiwa ni rekodi ya Mchezaji wa mbele kucheza mechi nyingi Timu ya England.
Wachezaji Carlton Cole wa West Ham na James Milner wa Aston Villa pia wamo kikosi hicho ikiwa ni mara yao ya kwanza kuitwa Timu ya Taifa.
Wayne Rooney wa Manchester United hayumo kwenye kikosi hicho kwa kuwa alikuwa majeruhi.
Vikosi vya Timu hizo ni kama ifuatavyo:
England:

Makipa: Robert Green (West Ham), Joe Hart (Man City), David James (Portsmouth).
Walinzi: Wayne Bridge (Man City), Ashley Cole (Chelsea), Rio Ferdinand (Man Utd), Phil Jagielka (Everton), Glen Johnson (Portsmouth), John Terry (Chelsea), Matthew Upson (West Ham), Luke Young (Villa).
Viungo: David Beckham (LA Galaxy), Gareth Barry (Villa), Michael Carrick (Man Utd), Stewart Downing (Middlesbrough), Frank Lampard (Chelsea), James Milner (Villa), Shaun Wright-Phillips (Man City), Ashley Young (Villa).
Washambuliaji: Gabriel Agbonlahor (Villa), Carlton Cole (West Ham), Peter Crouch (Portsmouth), Emile Heskey (Villa).
Spain:
Makipa: Iker Casillas (Real Madrid), Pepe Reina (Liverpool).
Walinzi: Raul Albiol (Valencia), Carlos Marchena (Valencia), Alvaro Arbeloa (Liverpool), Joan Capdevila (Villarreal), Juan Gutierrez (Real Betis), Gerard Pique (Barcelona), Carles Puyol (Barcelona), Sergio Ramos (Real Madrid).
Viungo: Xabi Alonso (Liverpool), Albert Riera (Liverpool), Sergi Busquets (Barcelona), Santiago Cazorla (Villarreal), Marcos Senna (Villarreal), Xavi Hernandez (Barcelona), Andres Iniesta (Barcelona), David Silva (Valencia).
Washambuliaji: Daniel Guiza (Fenerbahce), Fernando Llorente (Athletic Bilbao ), Fernando Torres (Liverpool), David Villa (Valencia).

No comments:

Powered By Blogger