Tuesday 10 February 2009

Harakati za Chelsea kutafuta Mrithi wa Scolari: Meneja wa Timu ya Taifa ya Urusi Guus Hiddink aanza mazungumzo na Chelsea!!

Guus Hiddink [62], raia wa Uholanzi [pichani], ambae kwa sasa ni Meneja wa Timu ya Taifa ya Urusi, amefuatwa na Klabu ya Chelsea, iliyomtimua Meneja wake Mbrazil Luiz Felipe Scolari hapo jana, ili kuiongoza hadi mwishoni mwa msimu huu.
Guus Hiddink ambae ana uhusiano wa karibu na Mmiliki wa Chelsea tajiri wa Kirusi Roman Abramovich na ambae ndie aliesababisha Hiddink apewe kazi ya Umeneja wa Urusi mwaka 2006, amesema: 'Ingekuwa Klabu nyingine nisingesita kusema hapana lakini Chelsea ni tofauti kwa sababu ya uhusiano wangu mzuri na mwenye mali.'
Chelsea imeshapewa kibali na FUR ambacho ndicho Chama cha Mpira cha Urusi kuzungumza na Guus Hiddink na habari hizi zimethibitishwa na Tovuti ya Chelsea.
Roman Abramovich ndie mfadhili mkuu wa FUR na pia anaekiendesha Chuo cha Mafunzo ya Soka huko Urusi.
Chelsea imetamka makubaliano yakifikwa basi Guus Hiddink atakuwa hapo klabuni hadi mwisho wa msimu lakini vilevile ataendelea kuwa Meneja wa Urusi.
Kwa sasa Chelsea iko chini ya usimamiza wa Meneja Msaidizi Ray Wilkins.
Guus Hiddink ameshawahi kuwa Kocha wa PSV Eindhoven, Real Madrid pamoja na Timu za Taifa za Netherlands, South Korea and Australia.

Sir Alex Ferguson ataja Kikosi chake kilichosajiliwa UEFA Champions League

Meneja wa Mabingwa wa England, Ulaya na Dunia Manchester United, Sir Alex Ferguson, ametaja Kikosi cha Wachezaji 30 waliosajiliwa kwa UEFA kwa ajili ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 inayoanza kuchezwa wiki mbili zijazo.
Kufuatana na Kanuni za UEFA, Kikosi cha Wachezaji 30 kinakuwa na Makundi mawili ya Wachezaji na la kwanza huitwa 'Listi A' ambayo ndiyo listi kuu na huwa na Wachezaji 25.
'Listi B' ni ile ya nyongeza ambayo ina majina ya Wachezaji watano waliozaliwa tarehe 1 Januari 1987 au baada ya hapo.
Mabadiliko kwenye Listi A ya Man U ni kukosekana kwa Owen Hargreaves ambae ni majeruhi na Manucho kwa sababu yuko Hull City kwa mkopo.
Nafasi zao zimechukuliwa na Federico Macheda na Davide Petrucci wote wakiwa Wachezaji chipukizi toka Timu ya Akiba ya Man U.
Mchezaji mpya aliesajiliwa Januari kutoka Serbia Zorin Tosic hayumo kwa sababu haruhusiwi kucheza kwa vile alishaechezea Klabu yake ya zamani Partizan Belgrade kwenye UEFA Champions League msimu huu pale walipofungwa na Fenerbahce kwenye Raundi ya 3.
Listi A [Na Namba zao za Jezi]:
Makipa: 1. Van der Sar, 12. Foster, 29. Kuszczak
Walinzi: 2. Neville, 3. Evra, 5. Ferdinand, 6. Brown, 15. Vidic, 20. Fabio, 21. Rafael, 22. O'SheaViungo: 8. Anderson, 11. Giggs, 13. Park, 16. Carrick, 17. Nani, 18. Scholes, 24. Fletcher, 34. Possebon, 43. Petrucci
Washambuliaji: 7. Ronaldo, 9. Berbatov, 10. Rooney, 32. Tevez, 41. Macheda
Listi B: Ben Amos, Richard Eckersley, Jonny Evans, Darron Gibson and Danny Welbeck.

No comments:

Powered By Blogger