Tuesday 10 February 2009

Wakala wa Scolari adai: 'Ametimuliwa na Mwenye Mali Abramovich!!'
Ferguson astushwa, asema ni alama za nyakati!!


Baada ya Luiz Felipe Scolari kufukuzwa na Chelsea kama Meneja na kazi hiyo kupewa kwa muda Ray Wilkin aliekuwa msaidi wake, Wakala wa Scolari ametangaza uamuzi wa kumtimua umefanywa na Mmiliki wa Chelsea, Roman Abramovich ambae alikerwa sana na mwendo mbaya wa Chelsea.
Chelsea mpaka sasa wako nafasi ya 4 kwenye LIGI KUU England wakiwa pointi 7 nyuma ya vinara Man U na wamecheza mechi moja zaidi ya Man U.

Hata hivyo, Chelsea bado wamo kwenye vindumbwembwe wa Vikombe vya FA na UEFA Champions League.
Jumamosi walitoka sare 0-0 nyumbani kwao Stamford Bridge na Timu 'dhaifu' Hull City na kundi la Mashabiki lilimzomea Scolari na kubwata: 'Hajui afanyalo!' huku baadhi wakiinua bango kubwa lililoandikwa: 'Mfukuzeni kazi!'.
Msimu huu, Chelsea wamekuwa na rekodi mbaya kwenye LIGI KUU hasa walipocheza na vigogo wenzao kwani walifungwa nyumbani na ugenini na Liverpool, wakafungwa na Arsenal hapo kwao Stamford Bridge, wametoka suluhu Stamford Bridge na Man U lakini wakabamizwa bao 3-0 na Man U kwenye marudiano huko Old Trafford.
Wakala wa Scolari, Acaz Felleger, amesema: 'Uamuzi ni wa Abramovich. Scolari hakuwa kwenye nafasi nzuri ingawa Bodi na Wachezaji walikuwa wakimsapoti. Alirithi kikosi cha Wachezaji 'wazee' na juhudi zake za kuleta damu changa zilishindikana!'
Nae Sir Alex Ferguson, Meneja wa Manchester United ambae ndie anashikilia rekodi ya kudumu muda mrefu kazini kwa kuwepo zaidi ya miaka 22 na kuwa na mafanikio makubwa, amenena: 'Nimesikitika! Nimestuka sana! Hii ni alama ya nyakati! Dunia haina tena uvumilivu! Huyu amekuwa na timu miezi 7 tu na ukweli ni kwamba ni mwezi uliokwisha tu ndio timu ililegalega. Tatizo ni kuwa Chelsea wana matumaini makubwa sana!'
Tangu Roman Abramovich ainunue Chelsea mwaka 2003, Mrusi huyo tajiri sana ameshawatimua Mameneja wannne, wa kwanza alikuwa Claudio Ranieri mwaka 2004, akafuata Jose Mourinho Septemba 2007, kisha Avram Grant Mei 2008 na jana Scolari.

RATIBA MECHI ZA KESHO:

Jumatano, 11 Februari 2009
MECHI ZA KIMATAIFA ZA KIRAFIKI
Andorra v Lithuania,
Austria v Sweden,
Belgium v Slovenia,
Cameroon v Guinea,
Colombia v Haiti,
Egypt v Ghana,
Estonia v Kazakhstan,
FYR Macedonia v Moldova,
France v Argentina, [SAA 5 USIKU]
Germany v Norway,
Greece v Denmark,
Iceland v Liechtenstein,
Israel v Hungary,
Latvia v Armenia,
Morocco v Czech Republic,
Nigeria v Jamaica,
Portugal v Finland,
Romania v Croatia,
South Africa v Chile,
Spain v England, [SAA 6 USIKU]
Switzerland v Bulgaria,
Tunisia v Netherlands,
Turkey v Ivory Coast,
Venezuela v Guatemala,
Wales v Poland,

No comments:

Powered By Blogger