Thursday 12 February 2009

Spain 2 England 0

Jana England ilichapwa mabao 2-0 na Spain kwenye mechi ya kirafiki iliyochezwa nchini Spain.
Mabao ya Spain yalifungwa na David Villa dakika ya 36 na Llorente dakika ya 82.
David Beckham aliingizwa dakika ya 46 na hiyo ikawa ni mechi yake ya 108 kuichezea England ikiwa ni sawa na rekodi iliyokuwa inashikiliwa na Bobby Moore kucheza mechi nyingi.

MATOKEO MECHI NYINGINE ZA KIRAFIKI:

France 0 Argentina 2
Germany o Norway 1
Portugal 1 Finland 0
Tunisia 1 Holland 1
Tanzania 0 Zimbabwe 0
Brazil 2 Italy 0

Chelsea wathibitisha Hiddink Meneja mpya

Chelsea imetangaza Guus Hiddink ndie Meneja mpya atakaechukua nafasi ya Luiz Felipe Scolari alietimuliwa.
Hiddink ataendelea pia kuwa Meneja wa Timu ya Taifa ya Urusi na inaaminika nafasi yake hapo Chelsea ni mpaka mwisho wa msimu huu.


Adebayor MCHEZAJI BORA AFRIKA

Mshambuliaji wa Togo na Arsenal Emmanuel Adebayor ametunukiwa na CAF, Chama cha Soka cha Afrika, tuzo ya MCHEZAJI BORA AFRIKA 2008.K
Ameshinda tuzo hiyo baada ya kura iliyopigwa miongoni mwa Makocha wa Timu za Taifa za Afrika na Adebayor alipata pointi 74 na mpinzani wake mkubwa Mohammed Aboutrika wa Misri alipata pointi 53.

Washindi wa Tuzo nyingine za CAF ni:

Mchezaji Bora wa Klabu: Aboutrika [AL AHLY]
Timu Bora ya Taifa: Misri
Klabu Bora: Al Ahly
Mchezaji Bora Kijana: Salomon Kalou
Mchezaji Bora Wanawake: Alice Mattlou [Afrika Kusini]
Kocha Bora: Hassan Shehata

Meneja Newcastle Kinnear kufanyiwa operesheni ya moyo

Joe Kinnear [62] Meneja wa Newcastle ambae yuko hospitalini tangu Jumamosi inabidi afanyiwe opersheni ya moyo na huenda akaukosa msimu wote uliobaki.
Kinnear alichukua hatamu hapo Newcastle Septemba 2008 baada ya Kevin Keagan kutimka.

No comments:

Powered By Blogger