Sunday 8 February 2009

Veterani Giggs afunga goli tamuuu, Man U wavunja rekodi Dakika 1193 bila nyavu zao kutikiswa na hizo ni Mechi 13!!

Mabingwa Manchester United wamerudi tena kileleni baada ya kushinda ugenini Upton Park bao 1-0 na kuwaliza wenyeji West Ham timu ambayo wakiwa hapo kwao kawaida huwatoa nishai Man U.
Ni veterani Ryan Giggs aliefunga goli tamu sana dakika ya 61 kufuatia kona aliyopiga mwenyewe na kuokolewa na West Ham lakini ikamkuta Paul Scholes katikati ya uwanja na akatoa pasi ndefu kwa Giggs aliekuwa wingi ya kushoto aliempiga chenga Carlton Cole na kumhadaa Noble kisha akapiga shuti kwa mguu wake dhaifu wa kulia na kufunga goli ambalo bila shaka linaweza kuwemo kwenye listi ya magoli bora ya msimu!

Kwa ushindi huu ambao hawakufungwa goli sasa Man U wamevunja rekodi ya Uingereza kwa kucheza muda mrefu bila nyavu zao kuguswa ikiwa ni dakika 1193 sawa na mechi 13!
Sasa Man U wana pointi 56 kwa mechi 24, huku Liverpool ni wa pili akiwa na pointi 54, Villa wa tatu pointi 51 akifuata Chelsea pointi 49 na Arsenal ni wa 5 pointi 44 timu zote hizi zikiwa zimecheza mechi 25, mechi moja zaidi ya Man U.
Vikosi vilivyoanza:
West Ham:
Green, Neill, Collins, Upson, Ilunga, Behrami, Parker, Noble, Collison, Cole, Di Michele.
Akiba: Lastuvka, Nsereko, Boa Morte, Kovac, Spector, Tristan, Sears.
Man Utd: Van der Sar, Rafael Da Silva, Ferdinand, Vidic, O'Shea, Ronaldo, Scholes, Carrick, Giggs, Tevez, Berbatov.
Akiba: Foster, Park, Nani, Welbeck, Fabio Da Silva, Fletcher, Eckersley.

Mtu 10 Arsenal wajitutumua na kutoka droo na Tottenham!!
Nyota Adebayor aumia kuwa nje wiki 6!!!!


Arsenal wakiwa ugenini White Hart Lane nyumbani kwa majirani na mahasimu wao wakubwa Tottenham wamefanikiwa kutoka sare ya 0-0 huku wakicheza watu 10 tu kwa muda mwingi wa gemu hii baada ya Mchezaji wao Eboue kutolewa nje dakika ya 38 ya kipindi cha kwanza kufuatia kupewa Kadi ya pili ya Njano baada ya kumkwatua Luka Modric.
Eboue alipewa Kadi ya kwanza ya Njano dakika ya 19 ya mchezo kwa kumletea ubishi Refa Mike Dean.
Ingawa Tottenham walitawala mchezo walishindwa kuipasua ngome ya Arsenal iliyoongozwa vizuri na Gallas na Kolo Toure huku Kipa Alumnia akiwa makini sana.
Katika mechi hii Mshambuliaji Staa wa Arsenal Adebayor, alieumia musuli ya nyuma ya paja kwenye dakika ya 38 na akaingizwa Bendtener, atakuwa nje kwa wiki 6 habari zilizothibitishwa na Meneja Arsene Wenger.

Hivyo Adebayor atazikosa mechi za Arsenal dhidi ya Cardiff, ikiwa mechi ya marudiano Kombe la FA, mechi za LIGI KUU dhidi ya Sunderland na Fulham, na ile ya UEFA Champions League watakayocheza na AS Roma.
Vikosi vilivyoanza vilikuwa:
Arsenal wanabaki nafasi ya 5 wakiwa na pointi 44 pointi 5 nyuma ya Timu ya 4 Chelsea na pointi 10 nyuma ya Liverpool inayoongoza ligi.
Tottenham wako nafasi ya 15.
Tottenham: Cudicini, Corluka, Dawson, Woodgate, Assou-Ekotto, Lennon, Jenas, Palacios, Modric, Pavlyuchenko, Keane.
Akiba: Gomes, Bale, Zokora, Huddlestone, Bent, Taarabt, Chimbonda.
Arsenal: Almunia, Sagna, Toure, Gallas, Clichy, Eboue, Song Billong, Denilson, Nasri, Adebayor, Van Persie.
Akiba: Fabianski, Eduardo, Ramsey, Djourou, Arshavin, Bendtner, Gibbs.

Benitez ang'ang'ania uteuzi wake wa Timu ni sawa tu!!

Washabiki wengi wa Liverpool na hata watu wa pembeni mara nyingi hushangazwa na jinsi Meneja wa Liverpool Rafael Benitez anavyopanga Timu yake.
Jana haikuwa tofauti wakati, kwa mara nyingine tena, alipowashangaza wengi kwa kuwaacha nyota kama Dirk Kuyt na Fernando Torres kwenye mechi ya jana na Portsmouth na kuuamua tu kuwaingiza dakika za mwisho wakati Liverpool ishafungwa na Wachezaji hao hawakufanya ajizi wakafunga mabao yaliyowapa ushindi wa 3-2.
Mwenyewe Benitez anatetea: 'Torres ni mmoja kwenye kikosi na wapo wengine wanaofanya timu iwe imara! Tungefungwa lakini tumeshinda!!'


Wilkins amtetea Scolari!!

Meneja msaidizi wa Chelsea, Ray Wilkins, amejitokeza kumtetea Bosi wake Luiz Felipe Scolari ambae jana alizomewa na Mashabiki wa Chelsea uwanjani kwao Stamford Bridge mara baada ya kutoka suluhu ya 0-0 na Hull City kwenye mechi ya LIGI KUU.
Mashabili hao walizomea huku wakibwata:'Hujui unachokifanya!'
Wilkins amesema: 'Wakitaka kuzomea shauri yao lakini wasiseme hajui anachokifanya kwani Scolari ana mafanikio makubwa kwenye soka.'
Scolari aliiongoza Brazil kutwaa Kombe la Dunia mwaka 2002 lakini tangu atue hapo Chelsea imeshapoteza pointi 16 hapo Stamford Bridge kwenye LIGI KUU wakati hapo kulikuwa ndio ngome yao kuu.
Baadhi ya Mashabiki kwenye mechi hiyo ya jana waliinua bango kubwa lililoitaka Chelsea imfukuze kazi Scolari. Bango hilo lilionyeshwa pale Scolari alipofanya uamuzi wa kumbadilisha Mchezaji mpya Ricardo Quaresma na kumwingiza Didier Drogba.

No comments:

Powered By Blogger