Friday 13 February 2009

Kutoka Urusi na.......mapenzi!!!!

Meneja wa Timu ya Taifa ya Urusi na ambae pia ndie Meneja mpya wa Chelsea, Guus Hiddink [pichani na tajiri Abramovich], anaamini Chelsea bado wana nafasi nzuri kwani bado wamo kwenye mapambano ya kugombea Vikombe vitatu.
Hiddink amesema: 'Kuna Kombe la FA, Kuna Ubingwa wa Ulaya na ipo LIGI KUU! Ndio tuko pointi 10 nyuma kwenye ligi lakini lolote linaweza kutokea!'
Guus Hiddink mwenyewe amekiri bila ya uswahiba mkubwa na mmiliki wa Chelsea, Roman Abramovich, ambae pia ndie mfadhili mkubwa wa soka ya Urusi, asingekubali kwenda Chelsea.
Inaaminika kazi ya ukocha wa Urusi Guus Hiddink amepewa na Abramovich na inasadikiwa Mrusi huyo tajiri ndie anaemlipa mshahara wa kuwa Meneja wa Urusi.
Hakika, NI KUTOKA URUSI.........NA MAPENZI!!!!!!

Giggs asaini mkataba mpya Man U!!

Ryan Giggs [35] amesaini nyongeza ya mwaka mmoja kwenye mkataba wake ambao sasa utamweka Manchester United hadi msimu ujao utakapoisha katikati ya mwaka 2010.
Winga veterani Giggs, ambae ameshachezea mechi 787 hapo Man U ikiwa ni rekodi kwa Mchezaji kucheza mechi nyingi klabuni hapo, alianza kuwachezea Mabingwa hao mwaka 1991.
Giggs ndie Mchezaji alieshinda Vikombe vingi hapo Man U kupita mwingine yeyote na ameshachukua Ubingwa wa LIGI KUU England mara 10, UEFA Champions League mara 2, FA Cup mara 4 na Kombe la Ligi [sasa linaitwa Carling Cup] mara 2.
Goli lake la ushindi Jumamosi iliyopita wakati Man U walipowafunga West Ham 1-0 kwenye LIGI KUU limemfanya awe Mchezaji pekee aliefunga bao kila msimu kwa misimu 17 mfululizo tangu LIGI KUU England ianzishwe.

Straika Mahakamani kwa 'Shambulio la Ngono'!!

Mshambuliaji wa Wigan, Marlon King [28], ambae yupo kwa mkopo Middlesbrough atafikishwa Mahakamani tarehe 25 Februari 2009 akishtakiwa kosa la 'Shambulio la Ngono' na kumjeruhi mwanamke mwenye umri wa miaka 20 kwenye Baa moja huko Soho jijini London.
Tukio hilo inasemekana lilitokea Desemba 7 mwaka jana na kusababisha mwanamke huyo avunjike pua na kupasuka mdomo.
Marlon King pia ni Mcchezaji wa Timu ya Jamaica.

No comments:

Powered By Blogger