Saturday 7 February 2009

Liverpool wachukua uongozi 'kwa muda', Villa wa tatu, Chelsea adoda!!!

Liverpool sasa anaongoza LIGI KUU England, pengine mpaka kesho tu, baada ya kupata ushindi wa ajabu kwa kupata mabao ya kushangaza walipocheza na timu inayodidimia Portsmouth.
Liverpool walipata bao la tatu dakika za mwisho likifungwa na Nyota Fernando Torres aliengizwa mwishoni na kuwapa ushindi wa 3-2.
Portsmouth walikuwa wakiongoza kwa bao 2-1 hadi dakika 5 zikisalia lakini Kuyt akasawazisha na Torres akawaua Portsmouth dakika za majeruhi.
Liverpool yuko kinarani akiwa na pointi 54 kwa mechi 25, wa pili ni Man U pointi 53, mechi 23 huku Chelsea aliebanwa leo na Hull City kwa kutoka sare ya 0-0, akiporomoka hadi nafasi ya 4.
Aston Villa kwa kuifunga leo Blackburn 2-0 wamepanda hadi nafasi ya 3 wakiwa na pointi 51 kwa mechi 25.
Chelsea ana pointi 49, mechi 25.
Arsenal wapo nafasi ya 5 na wana pointi 43 na wanacheza kesho ugenini na jirani na mahasimu wao, watoto wa jiji moja London, tena London ya Kaskazini, Tottenham ambao watakuwa kwao White Hart Lane.
Timu hizi kwenye mzunguko wa kwanza wa LIGI KUU walitoka 4-4.
Mabingwa Man U watakuwa Upton Park nyumbani kwa West Ham na wakitoka sare tu watachukua tena uongozi wa ligi huku wakiwa na mechi moja mkononi.

MATOKEO YA MECHI ZOTE:

Blackburn 0-2 Aston Villa
Chelsea 0-0 Hull
Everton 3-0 Bolton
Man City 1-0 Middlesbrough
Portsmouth 2-3 Liverpool
Sunderland 2-0 Stoke
West Brom 2-3 Newcastle
Wigan 0-0 Fulham

No comments:

Powered By Blogger