Monday 2 February 2009

Refa Mike Riley 'aihujumu' Chelsea!!!!

Kadi Nyekundu, ambayo Timu nzima ya Chelsea ililalamikia, kwa Kiungo Frank Lampard kwenye dakika ya 60 iliwakata maini na kuruhusu Liverpool kuwachosha Chelsea na kupata mabao 2 dakika za mwishoni.
Lampard waziwazi kabisa aliucheza mpira lakini Refa Mike Riley akadhani amemchezea Rafu mbaya Xabi Alonso.
Uamuzi huu uliidhoofisha sana Chelsea mbayo tayari ilionekana kuzidiwa kila kitu.
Torres alifunga bao la kwanza dakika ya 88 na la pili dakika za majeruhi.

Newcastle 1 Sunderland 1

Djibril Cisse aliipatia Sunderland dakika ya 32 lakini Refa Howard Webb aliwapa Newcastle penalti tata iliyofungwa na Shola Ameobi dakika ya 69.

No comments:

Powered By Blogger