Thursday 5 February 2009

FA CUP: Everton waibwaga Liverpool!!!

Everton wakiwa nyumbani kwao Goodison Park waliwatoa nje ya Kombe la FA Watani wao wa Jadi Liverpool kwa bao 1-0 bao alilofunga chipukizi wa miaka 19 Dan Gosling katika dakika 120 za muda wa nyongeza baada ya mechi kwisha 0-0 katika dakika 90.
Timu hizi zilitoka suluhu ya 1-1 katika mechi iliyochezwa Anfield wiki iliyokwisha na mechi hii ni marudiano.
Dan Gosling aliingizwa kama Mchezaji wa Akiba na alipachika bao la ushindi dakika ya 118 zikiwa dakika mbili tu kabla gemu haijaenda tombola ya penalti.
Liverpool ilishusha kikosi chake kamili kilichombamiza Chelsea lakini walipata pigo kubwa dakika ya 16 tu baada ya Nahodha na 'Mbeba Timu' Steve Gerrard kuumia na kutolewa na inasadikiwa atakuwa nje kwa wiki hadi 4.
Pigo jingine kwa Liverpool ni pale Leiva Lucas alipolambwa Kadi Nyekundi kipindi cha pili baada ya kupewa Njano mbili.
Kwenye mechi yote hii Mfungaji wao stadi Fernando Torres alionekana ni abiria tu na ilibidi atolewe aingizwe Babel.
Sasa Everton wamesonga mbele na watacheza na Aston Villa Raundi ya 5 ya Kombe hili la FA.


MATOKEO MECHI NYINGINE ZA LEO ZA MARUDIANO NI:
Aston Villa 3-1 Doncaster
Blackburn 2-1 Sunderland [BAADA YA DAKIKA 120]
Nottm Forest 2-3 Derby

RATIBA YA MECHI ZA RAUNDI YA 5:

Jumamosi, 14 Februari 2009
[SAA 9:45 MCHANA]
Swansea v Fulham
[SAA 12 JIONI]
Sheffield United v Hull
Blackburn v Coventry
West Ham v Middlesbrough
[SAA 2:30 USIKU]
Watford v Chelsea
Jumapili, 15 Februari 2009
[SAA 11:30 JIONI]

Everton v Aston Villa
[SAA 1:30 USIKU]
Derby v Man U
Jumatatu, 16 Februari 2009
[SAA 4:45 USIKU]

Arsenal v Cardiff [Marudiano ya Raundi ya 4 Mshindi anacheza na Burnley kwenye Raundi ya 5]

No comments:

Powered By Blogger