Monday 2 February 2009

Robbie Keane arudi Tottenham!!!

Tottenham imemsaini tena aliekuwa Nahodha wao miezi 6 tu tangu wamuuze kwa Liverpool kwa Pauni Milioni 20.3 na safari hii dau la kuuzwa kwa Keane na Liverpool halikutajwa lakini inaaminika ni Pauni Milioni 15.
Robbie Keane akiwa hapo Liverpool alicheza mechi 19 na kufunga mabao matano.
Keane ambae alikuwa Tottenham tangu Agosti 2002 hadi Julai 2008 alicheza mechi 254 na kufunga mabao 107 hapo Tottenham.
Keane ni Mchezaji wa tatu aliewahi kuchezea Tottenham na kurudishwa tena hapo na Meneja Harry Redknapp ndani ya huu mwezi mmoja wengine wakiwa Jermaine Defoe alierudi toka Portsmouth na Pascal Chimbonda kutoka Sunderland.

Dili ya Arshavin kwenda Arsenal hatihati, N'Zogbia yuko Wigan na Dacourt arudi tena England!!

Huku muda ukiyoyoma na dirisha likikaribia kubamizwa komeo, ile vuta nikuvute kati ya Arsenal na Klabu ya Kirusi Zenit St Petersburg kuhusu uhamisho wa Andrei Arshavin inaendelea.
Taarifa zinasema huenda dili hiyo imekufa baada ya pande zote mbili kushindwa kukubaliana dau la uhamisho na nini walipwe hao Warusi kama fidia kwa Nyota Arshavin aliewika kwenye EURO 2008 kuvunja mkataba na Klabu yake Zenit.
Klabu za Wigan na Newcastle zimekubaliana kubadilishana Wachezaji huku Mlinzi Ryan Taylor [24] akienda Newcastle na Charles N'Zogbia akitoka Newcastle kwenda Wigan ingawa Wigan imebidi pia watoe Pauni Milioni 6 ili kumchukua N'Zogbia.
N'Zogbia alijiunga Newcastle kutoka Le Havre ya Ufaransa mwaka 2004 na Taylor alijiunga na Wigan mwaka 2006 kutoka Tranmere.
Nae Mchezaji wa Kimataifa wa Ufaransa, Olivier Dacourt [34], aliewahi kuchezea LIGI KUU akiwa na Everton na Leeds, ametua Fulham kwa mkopo akitokea Inter Milan.

No comments:

Powered By Blogger