Friday 6 February 2009

Mchezaji mwingine wa Man City mbaroni!!!

Baada ya Robinho kujikuta mikononi mwa Polisi na huku uchunguzi wa kesi yake ya 'shambulio la ngono' ukiendelea, Mchezaji mwingine wa Manchester City amejikuta mikononi mwa Polisi wa Manchester baada kutokea ugomvi nje ya Naiti Klabu siku ya Mkesha wa Krismas.
Mchezaji huyo ni Mlinzi Micah Richards [20] ambae alihojiwa na Polisi na kuachiwa kwa dhamana mpaka tarehe 8 Aprili 2009 huku uchunguzi ukiendelea.


Steven Gerrard nje wiki 6!!!

Nahodha na 'Mbeba Timu' wa Liverpool, Steven Gerrard, atakuwa nje ya uwanja kwa wiki 3 baada ya uchunguzi kuthibitisha amechanika musuli mguuni.
Gerrard aliumia na kutolewa kwenye dakika ya 16 tu ya mechi kuwania Kombe la FA ambayo Liverpool alifungwa 1-0 na mahasimu wao wakubwa Everton.
Gerrard atazikosa mechi za Liverpool dhidi ya Portsmouth, Man City na hata ile ya UEFA Champions League na Real Madrid hapo Februari 25. Pia ataikosa mechi ya kirafiki ya England watakapocheza na Spain wiki ijayo.

No comments:

Powered By Blogger