Saturday 7 February 2009

MECHI ZA LIGI KUU:

Jumamosi, 7 Februari 2009

Man City v Middlesbrough [saa 9 dak 45 mchana]
[saa 12 jioni]
Blackburn v Aston Villa
Chelsea v Hull
Everton v Bolton
Portsmouth v Liverpool
Sunderland v Stoke
West Brom v Newcastle
Wigan v Fulham

Jumapili, 8 Februari 2009

[saa 10 na nusu jioni]
Tottenham v Arsenal

[saa 1 usiku]
West Ham v Man U

Endapo leo Liverpool, anaesafiri kwenda Portsmouth, atawafunga wenyeji wao hao ambao wako nafasi ya 16 kwenye msimamo wa ligi ikiwa ni pointi moja tu juu ya timu zilizo nafasi ya kushuka daraja, basi atachukua uongozi wa LIGI KUU kwa kumpita Manchester United ambae mechi yake inachezwa kesho.
Hata hivyo, Liverpool atakuwa amecheza mechi 2 zaidi ya Man U.
Ushindi kwa Liverpool ni muhimu hasa kufuatia kipigo cha Jumatano walichopewa na mahasimu wao wakubwa Everton kwa bao 1-0 na kuwatoa nje ya Kombe la FA.
Katika mechi hiyo Liverpool walipata pigo kubwa baada ya Nahodha wao Steven Gerrard kuumia na sasa atakuwa nje ya kwa wiki 3.
Wengi wanajua bila ya Gerrard Liverpool inapwaya mno na ndio maana macho ya wengi yapo kwenye mechi hii.
Kwa upande mwingine, Portsmouth wakiwa chini ya Meneja Tony Adams, Nahodha wa zamani wa Arsenal, wako taabani wakiwa wamepata pointi moja katika mechi 7 za LIGI KUU zilizopita na hii ni presha kubwa kwa Tony Adams kutimuliwa.
Leo, Timu iliyo nafasi ya 3, nyuma ya Liverpool, Chelsea, inawakaribisha Hull City na ikiwa watashinda na Liverpool kufungwa mechi yake ya leo, basi watafungana kwa pointi na Chelsea atakuwa juu ya Liverpool kwa ubora wa tofauti ya magoli.

Ferguson na Vidic watwaa Tuzo ya Barclays kwa Januari!!!

Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, na Beki wake, Nemanja Vidic, wamepewa Tuzo za Barclays za Meneja na Mchezaji bora wa Januari kwa kila mmoja na hii ikiwa ni mara ya kwanza kwa Vidic kutunukiwa tuzo hiyo lakini ni mara ya 22 kwa Sir Alex Ferguson kushinda.
Barclays ndio wadhamini wakuu wa LIGI KUU England na wamewazadia Manchester United kwa kushinda mechi zao zote 5 za LIGI KUU kwa mwezi Januari bila ya kufungwa hata goli moja.
Man U walianza Januari kwa kuziwasha Chelsea 3-0 na West Brom 5-0 na kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Wigan, Bolton na Everton.
Kwa sasa Man U ndie kinara wa ligi.

Materazzi ashinda kesi, alipwa Mamilioni ya Pauni kama Fidia!!!

Marco Materazzi, Mtaliani aliejizolea umaarufu wa kuchukiwa, hasa baada ya Fainali ya Kombe la Dunia mwaka 2006 kati ya Italy na France pale 'alipokula ndosi' na kusababisha kipenzi Zinedine Zidane 'aone Nyekundu', ameshinda kesi yake Mahakama Kuu England na sasa Gazeti la SUN itabidi limlipe fidia ambayo inaaminika ni Mamilioni ya Pauni.
Gazeti hilo inasemekana lilidai Materazzi alimwambia Zidane ni 'mtoto wa malaya wa haramia' na ndio maana Zidane, ambae asili yake ni Mwarabu wa Algeria, alikasirika na kumtwanga kichwa ambacho Refa hakuona ila tukio hilo lilionwa na Refa wa Akiba aliembonyeza mwenzake na kumpa Kadi Nyekundu.
Mechi hiyo ya Fainali Kombe la Dunia iliisha 1-1 lakini Italia waliibuka Mabingwa baada ya kushinda kwa tombola ya penalti.
Hii ni kesi ya 3 kwa Materazzi kuyashinda Magazeti ya England, mengine yakiwa Daily Star na Daily Mail, yote yakimlipa fidia kuhusu ishu ya Zidane.

N'Zogbia na Kinnear waendelea kuchambana magazetini!!!

Bosi wa Newcastle, Joe Kinnear na aliekuwa Mchezaji wake, Charles N'Zogbia, ambae sasa amehamia Wigan, wameendelea kuwakiana magazetini huku kila mmoja akimkandya mwenzake.
Vita hii iliianza kama wiki moja sasa na ndio ilisababisha N'Zogbia kudai ahamishwe na hatimaye kuhamia Wigan siku chache zilizopita.
Chanzo kilikuwa pale Joe Kinnear akiwa kwenye mahojiano na Waandishi wa Habari kurekodiwa akimwita Charles N'Zogbia 'Charles Insomnia', Imsomnia likiwa neno la Kiingereza lenye maana kukosa usingizi, kitu ambacho kilimkasirisha sana N'Zogbia ingawa Kinnear alijitetea alikosea tu kutamka jina hilo na hakuwa na nia ya dhihaka.
N'Zogbia, baada ya kuhama, ameibuka na kudai: 'Kinnear hana uwezo wa kuongoza Klabu. Ukimsikia Meneja akisema vitu vile ujue hakuheshimu na kama hana heshima kuna faida gani kucheza timu yake? Sikuwa na furaha kuchezea Newcastle, Meneja alikuwa haongei na mimi!!!'
Nae Kinnear amejibu: 'Maneno yake ni vichekesho!! Yeye alitaka kuhama tu na kila siku ananifuata mara Arsenal, mara Man U, mara Real wanamtaka na sasa kaishia Wigan!! Alikuwa kwenye dunia ya Abunuwasi!!'

No comments:

Powered By Blogger