Monday 2 February 2009

Dirisha la Uhamisho Wachezaji kufungwa leo saa 2 usiku [saa za bongo]!!!

Dirisha la Uhamisho Wachezaji litafungwa leo saa 2 usiku, saa za kibongo, ingawa kuna habari zisizothibitishwa huenda likasogezwa mbele kidogo ili kutoa nafasi zaidi kwa sababu Uingereza yote imekumbwa na hali mbaya ya hewa hasa kufuatia kuanguka barafu nyingi kulikovuruga usafiri nchi nzima.
Mara baada ya kufungwa dirisha hilo tutawaletea taarifa kamili za Wachezaji gani wamehama dakika hizi za mwisho kwani kuna taarifa nyingi kuhusu mbio za dakika za mwisho .


FA England imepokea rufaa ya Lampard wa Chelsea kupinga Kadi Nyekundu.

Chama cha Soka England, FA, kimethibitisha kupokea rufaa toka Klabu ya Chelsea inayohusu Kadi Nyekundu aliyopewa Frank Lampard na Refa Mike Riley kwenye mechi ambayo Chelsea alifungwa bao 2-0 na Liverpool uwanjani kwa Liverpool Anfiled katika mechi ya LIGI KUU hapo jana.
Ingawa Refa Mike Riley alikuwa kama mita 2 tu toka walipovaana Lampard na Alonso na ingawa marudio ya video yameonyesha Lampard aliucheza mpira na hakukusudia kucheza rafu, Refa huyo alitoa Kadi Nyekundu moja kwa moja.
Hii si mara ya kwanza kwa Lampard na Alonso kukwaana uwanjani kwani mwaka 2005 Lampard alimvunja enka Alonso.
Endapo rufaa ya Lampard itatupwa basi atazikosa mechi za LIGI KUU dhidi ya Hull na Aston Villa na ile ya Raundi ya 5 ya Kombe la FA dhidi ya Watford.
FA itaisikiliza Rufaa hiyo siku ya Jumanne ijayo.


MECHI ZIJAZO ZA LIGI KUU ENGLAND [saa ni za bongo]

Jumamosi, 7 Februari 2009
Man City v Middlesbrough [saa 9 dak 45 mchana]
[saa 12 jioni]
Blackburn v Aston Villa
Chelsea v Hull
Everton v Bolton
Portsmouth v Liverpool
Sunderland v Stoke
West Brom v Newcastle
Wigan v Fulham
Jumapili, 8 Februari 2009
[saa 10 na nusu jioni]
Tottenha v Arsenal
[saa 1 usiku]
West Ham v Man U
Jumamosi, 14 Februari 2009
[saa 12 jioni]

Portsmouth v Man City
Jumatano, 18 Februari 2009
[saa 5 usiku]

Man U v Fulham

No comments:

Powered By Blogger