Wednesday 4 February 2009

FA CUP: BURNLEY 3 WEST BROM 1

Katika mechi ya marudiano ya Raundi ya 4 ya Kombe la FA jana, timu ya daraja la chini Burnley imeiadhiri West Brom kwa kuinyuka mabao 3-1 na hivyo kuingia Raundi ya 5 na itakutana na mshindi kati ya Arsenal na Cardiff mechi iliyokuwa pia ichezwe jana lakini ikaahirishwa kwa sababu ya hali ya hewa kufuatia dhoruba ya barafu nyingi kuanguka Uingereza.
Sasa Arsenal na Cardiff watacheza Februari 16.

MECHI ZA MARUDIANO ZA FA CUP LEO 4 Februari 2009:

[Saa 4 dak 45 usiku]
Aston Villa v Doncaster
Nottingham Forest v Derby
[Saa 5 usiku]
Blackburn v Sunderland
Everton v Liverpool

Kadi Nyekundu ya Lampard yafutwa!!

Kadi Nyekundu aliyopewa Frank Lampard na Refa Mike Riley kwa kumchezea rafu Xabi Alonso wa Liverpool kwenye mechi ya Jumapili ilyopita ambayo Liverpool aliifunga Chelsea 2-0 imefutwa na FA baada ya Rufaa ya Chelsea.
Sasa Lampard yuko huru kucheza mechi zijazo.

PILIKAPILIKA ZA UHAMISHO ZILIVYOISHA!!

Baada ya dirisha la uhamisho kufungwa, chini ndio listi kamili ya biashara kamili iliyofanywa na Klabu za LIGI KUU ENGLAND.

Arsenal
Kuingia: Andrei Arshavin (Zenit St Petersburg,)
Kuhama: Gavin Hoyte (Watford mkopo); Jay Simpson (West Brom, mkopo)
Aston Villa
Kuingia:Emile Heskey (Wigan dau, £3.5m)
Kuhama: Wayne Routledge (QPR, £300,000)
Blackburn Rovers
Kuingia: Gael Givet (Marseille, mkopo); El-Hadji Diouf (Sunderland, £2m)
Kuhama:Matt Derbyshire (Olympiacos, mkopo); Robbie Fowler (huru); Eddie Norlan (Preston NE,); Sergio Peter (Sparta Prague,)
Bolton Wanderers
Kuingia: Ariza Makukula (Benfica, mkopo); Sebastien Puygrenier (Zenit St Petersburg, mkopo); Mark Davies (Wolves, )
Kuhama: Kevin Nolan (Newcastle, £4m); Ian Walker (huru); Heidar Helguson (QPR)
Chelsea
Kuingia: Ricardo Quaresma (Inter Milan, mkopo)
Kuhama: Carlo Cudicini (Tottenham, bure); Ben Sahar (De Graafschap, mkopo); Jack Cork (Wolves, mkopo); Wayne Bridge (Manchester City, £10m); Scott Sinclair (Birmingham, mkopo)
Everton
Kuingia: Jo (Manchester City mkopo)
Kuhama: Hamna
Fulham
Kuingia: Olivier Dacourt (Inter Milan, mkopo); Giles Barnes (Derby, mkopo)
Kuhama: Jimmy Bullard (Hull, £5m); Andranik Teymourian (Barnsley, mkopo); Leon Andreasen (Hannover, mkopo); Soel Ki-Hyeon (Al-Hilal, mkopo); Hameur Bouazza (Birmingham, mkopo); Lee Cook (QPR, £1.9m)
Hull City
Kuingia: Jimmy Bullard (Fulham, £5m); Kevin Kilbane (Wigan); Manucho (Manchester United, mkopo); Kamil Zayatte (Young Boys, £2.5m alikuwa akichezea kwa mkopo sasa amekuwa wa kudumu)
Kuhama: Stelios Giannakopolous (Larissa); Dean Windass (Oldham, mkopo); Marlon King (Middlesbrough)
Liverpool
Kuingia: Hamna
Kuhama: Robbie Keane (Tottenham); Jermaine Pennant (Portsmouth, mkopo)
Manchester City
Kuingia: Shay Given (Newcastle, £6m); Nigel De Jong (Hamburg, £19m); Craig Bellamy (West Ham, £14m); Wayne Bridge (Chelsea, £10m)
Kuhama: Jo (Everton, mkopo); Tal Ben Haim (Sunderland)
Manchester United
Kuingia:
Zoran Tosic na Adem Ljajic (wote Partizan Belgrade, dau halikutajwa); Ritchie de Laet (Stoke)
Kuhama: Manucho (Hull, mkopo)
Middlesbrough
Kuingia: Marlon King (Hull, mkopo)
Kuhama: Mido (Wigan, mkopo)
Newcastle United
Kuingia: Ryan Taylor (Wigan); Kevin Nolan (Bolton, £4m); Peter Lovenkrands (huru)
Kuhama: Shay Given (Man City); Charles N'Zoigbia (Wigan)
Portsmouth
Kuingia: Angelo Basinas (AEK); Theofanis Gekas (Werder Bremen); Jermaine Pennant (Liverpool, mkopo); Nadir Belhadj (Lens, alikuwa mkopo sasa wa amenunuliwa); Hayden Mullins (West Ham, bure); Pele (Porto, mkopo)
Kuhama: Jermaine Defoe (Tottenham, £15m); Lassana Diarra (Real Madrid, £20m); Ben Sahar (Chelsea, mwisho wa mkopo)
Stoke City
Kuingia: Mathew Etherington (West Ham); James Beattie (Sheffield United, £3.5m); Henri Camara (Wigan, mkopo)
Kuhama: Ritchie de Laet (Man U); Tom Soares (Charlton, mkopo), Liam Lawrence (Derby)
Sunderland
Kuingia:
Tal Ben Haim (ManCity, mkopo); Calum Davenport (West Ham, mkopo)
Kuhama: Michael Chopra (Cardiff, mkopo); El-Hadji Diouf (Blackburn, £4m); Roy O'Donovan (Blackpool, mkopo); Ross Wallace (Preston, £100k); Liam Miller (QPR); Pascal Chimbonda (Tottenham)
Tottenham Hotspur
Kuingia: Robbie Keane (Liverpool, £12m); Wilson Palacios (Wigan, £15m); Jermaine Defoe (Portsmouth, £15m); Carlo Cudicini (Chelsea, bure); Pascal Chimbonda)
Kuhama: Hossam Ghaly (Al Nasar); Paul Stalteri (huru); Kevin Price-Boateng (Borussia Dortmund, mkopo); Cesar Sanchez (Valencia, mkopo)
West Bromwich
Kuingia: Juan Carlos Menseguez (San Lorenzo); Youssouf Mulumbu (Paris St-Germain, mkopo); Pele (Porto, mkopo); Marc-Antoine Fortune (Nancy, mkopo); Jay Simpson (Arsenal, mkopo)
Kuhama: Sherjill MacDonald (Roeselare, mkopo)
West Ham
Kuingia: Savio Nsereko (Brescia, £10m)
Kuhama: Julien Faubert (Real Madrid, mkopo); Craig Bellamy (Man City, £14m); Calum Davanport (Sunderland, mkopo); Mathew Etherington (Stoke); Nigel Quashie (Wolves, mkopo); Lee Bowyer (Birmingham, mkopo); Hayden Mullins (Portsmouth, bure); Kyel Reid (Wolves, mkopo)
Wigan Athletic
Kuingia: Charles N'Zoigbia (Newcastle); Mido (Middlesbrough, mkopo); Ben Watson (Crystal Palace, £2m); Hugo Rodallega (Necaxa, £4.5m)
Kuhama: Ryan Taylor (Necwastle); Wilson Palacios (Tottenham); Kevin Kilbane (Hull),
Emile Heskey (Aston Villa, £3.5m); Marlon King (Middlesbrough, mkopo); Henri Camara (Stoke, mkopo)


No comments:

Powered By Blogger