Sunday 19 April 2009


LEO VITA ya Ndugu wawili: Gary na Phillip Neville!!!!!

Gary Neville na Phillip Neville ni mtu na mdogo wake, baba mmoja na mama mmoja.
Gary ni mkubwa kwa Phillip kwa miaka miwili. Gary alizaliwa mwaka 1975 na Phillip mwaka 1977.
Ndugu hawa wote ni Wachezaji wa Timu ya Taifa ya England na wanae Dada yao, mdogo kwao aitwae Tracy, ambae yumo kwenye Timu ya Taifa ya Wanawake ya England.
Wote walianza kucheza soka tangu wako watoto wakiwa Manchester United lakini Phillipi Neville akauzwa kwenda Everton mwezi Agosti mwaka 2005 na Gary akabaki Man U.
Kwa sasa Najodha wa Manchester United ni Gary Neville na Nahodha wa Everton ni Phillip Neville.
Na leo, ndani ya Uwanja maarufu wa Wembley, Manchester United na Everton zinacheza kwenye Nusu Fainali ya FA CUP na mshindi atakutana na Chelsea hapo Mei 30.
Na ndugu hao wawili, wakiwa Manahodha wa Timu zao, wanatarajiwa kuziongoza Timu zao kuingia na kupambana katika jukwaa maarufu na la kihistoria huko Uingereza na Dunia nzima- Wembley Stadium.

No comments:

Powered By Blogger