Wednesday 22 April 2009

VUTA NIKUVUTE LIVERPOOL, ARSENAL!!!!!

Andrey Arshavin ameifungia Arsenal mabao manne lakini hilo halikuweza kuwapa ushindi kwani mabao mawili kila mmoja kutoka kwa Fernando Torres na Yossi Benayoun yalifanya mechi hii iishe 4-4. Sasa Liverpool amechukua uongozi wa ligi ingawa yuko pointi sawa na Man U wote wakiwa na pointi 71 lakini Liverpool ana tofauti ya magoli bora. Hata hivyo Liverpool amecheza mechi 2 zaidi ya Man U.
Kesho Jumatano Manchester United anacheza kwake Old Trafford na Portsmouth.
Vikosi vilikuwa:
Liverpool:
Reina, Arbeloa, Carragher, Agger, Aurelio, Alonso, Mascherano, Benayoun, Kuyt, Riera, Torres. Akiba: Cavalieri, Dossena, Babel, Lucas, Ngog, El Zhar, Skrtel.
Arsenal: Fabianski, Sagna, Toure, Silvestre, Gibbs, Arshavin, Song Billong, Fabregas, Denilson, Nasri, Bendtner. Akiba: Mannone, Diaby, Eduardo, Vela, Walcott, Ramsey, Eboue.

No comments:

Powered By Blogger