Sunday 19 April 2009

Manchester United v Everton

Leo saa 12 jioni, saa za kibongo, Mabingwa wa England, Ulaya na Dunia, Manchester United, wanajimwaga Wembley Stadium, London, kuvaana na Timu nyingine ya LIGI KUU England, Everton kwenye Nusu Fainali ya Kombe la FA na mshindi atakutana na Chelsea iliyoifunga Arsenal hapo jana bao 2-1 kwenye Fainali itakayochezwa tarehe 30 Mei 2009. Mbali ya kuwakosa majeruhi wa muda mrefu, Owen Hargreaves, na Wes Brown [ingawa ameshaanza mazoezi], Man U wanategemewa kuwa na kikosi chao kamili wakiwemo Garry Neville na Rafael da Silva ambao wamepona hivi karibuni.
Leo, baada ya kukosa mechi iliyopita dhidi ya FC Porto iliyochezwa Jumatano, Paul Scholes, Park Ji-sung na Carlos Tevez wanategemewa sana kuanza hasa baada ya Meneja Sir Alex Ferguson kuahidi mabadiliko ili kupumzisha baadhi ya Wachezaji hasa ukitilia maanani Jumatano ijayo kuna mechi muhimu ya LIGI KUU dhidi ya Portsmouth.
Meneja wa Everton, David Moyes, inabidi aamue kama atamuanzisha Louis Saha ambae alikuwa anaugua tumbo kwani hatowezi kumchezesha Mshambuliaji Jo ambae haruhusiwi kucheza mashindano haya kwa vile alishacheza alipokuwa na Timu yake Manchester City. Jo yuko Everton kwa mkopo.
Majeruhi wa muda mrefu wa Everton ambao sasa wamepona na wanaweza kucheza ni pamoja na Mlinzi kutoka Nigeria Joseph Yobo na Mshambuliaji James Vaughan.
Vikosi vinategemewa kuwa
Man Utd: Van der Sar, Foster, Kuszczak, Neville, Evra, Ferdinand, Vidic, Rafael, Fabio, O'Shea, Evans, Ronaldo, Anderson, Scholes, Fletcher, Gibson, Carrick, Park, Nani, Giggs, Rooney, Tevez, Berbatov, Macheda.
Everton: Howard, Hibbert, Lescott, Jagielka, Baines, Osman, Pienaar, Neville, Rodwell, Fellaini, Cahill, Yobo, Saha, Vaughan, Nash, Gosling, Jacobsen, Van der Meyde, Castillo, Baxter.
Refa: Mike Riley


Wenger akiri wamefungwa kwa kuwa walishindwa kumdhibiti Drogba


Baada ya kipigo cha 2-1 cha jana, goli la ushindi likifungwa na Mshambuliaji Didier Drogba, Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amekiri: 'Drogba ni muuaji! Tulimrahisishia kazi lakini Drogba ni Mchezaji anaefunga magoli muhimu kwenye mechi kubwa! Huwa anajidondosha maksudi mara kwa mara lakini ni Mchezaji hatari!'

Ingawa amekiri Drogba ndie aliewaua, Wenger amesema Kipa wao Lucasz Fabianski haepuki lawama ingawa hakutaka kusisitiza hilo akiogopa kumvunja moyo hasa kwa kuwa Jumanne wana mechi ngumu watakapochuana na Liverpool kwenye LIGI KUU.

Na Meneja wa Chelsea, Guus Hiddink, akiwa na furaha kubwa, alimmiminia sifa nyingi Drogba na kusema huwezi kumtathmini Mshambuliaji kwa kufunga tu bali pia kwa kuhangaika kwake kuisaidia Timu kitu ambacho Drogba anakifanya kwa bidii sana.

Timu ya Ujerumani yaomba radhi kwa Mashabiki wake kwa kufungwa kwa kuwarudishia pesa zao za viingilio!!!!!

Baada ya kubandikwa mabao 4-0 ugenini kwenye mechi ya Bundesliga siku ya Ijumaa iliyopita huko Ujerumani walipokutana na Schalke, Timu ya Energie Cottbus imewataka radhi Mashabiki wake 600 waliosafiri umbali wa Kilomita 610 hadi Gelsenkirchen na kuambulia kuona Timu yao ikipata kipigo chake cha sita katika mechi 7. Cottbus ambao wako nafasi ya pili toka chini kwenye msimamo wa Bundesliga na wako hatari ya kuporomoka Daraja imetamka itarudisha pesa za viingilio kwa Mashabiki wake waliokwenda kuiona mechi hiyo ikiwa ni ishara ya kuomba msamaha.

MECHI ZA LEO: Jumapili, 19 Aprili 2009
LIGI KUU ENGLAND

[saa 9 na nusu mchana]Tottenham v Newcastle

[saa 11 jioni]Man City v West Brom

No comments:

Powered By Blogger