Thursday 23 April 2009

Scholes afikisha mechi 600 Man United!!

Kiungo wa Mabingwa Manchester United Paul Scholes, jana alipocheza katika mechi ya LIGI KUU England dhidi ya Portsmouth ambayo Man U walishinda mabao 2-0 na kupaa kileleni mwa ligi hiyo, amefikisha jumla ya mechi 600 kwenye Klabu hiyo na sasa yeye ni Mchezaji wa 4 katika safu ya Wachezaji wa Klabu hiyo waliocheza mechi nyingi katika historia yake. Ryan Giggs, ambae jana pia alicheza, ndie anaeongoza kwa mechi 799, Sir Bobby Charlton mechi 758 na Bill Foulkes mechi 658.
Scholes ni Mchezaji asie na makuu, mkimya sana na siku zote hapendi kutangazwa lakini watu humsifia kama alivofanya Mchezaji Bora wa zamani Duniani, Zinedine Zidane ambae aliwahi kusema: 'Ni Kiungo Bora Duniani katika Wachezaji wa rika lake!!'
Paul Scholes ambae sasa ana umri wa miaka 34 alianza kuichezea Man U tangu akiwa na miaka 19 na ameshafunga jumla ya mabao 142.
Rio Ferdinand anamwelezea: 'Tukiwa nae mazoezini huwa anafanya vitu vya ajabu ambavyo hakuna Mchezaji mwingine anaweza! Siku moja tukiwa mazoezini kwenye Kituo chetu Carrington, nadhani alikuwa Rooney, alikuwa anajisaidia pembeni mwa uwanja mita kama 80 toka tulipo. Scholes akachukua mpira na kutuonyesha alipo Rooney. Akafumua shuti umbali huo wa mita kama 80 na kumpiga Rooney na mpira!! Wote tukajaribu kulenga umbali ule na hakuna hata mmoja aliefanikiwa kupata shabaha!! Vitu kama hivyo anavifanya mara kwa mara tu!!!'
Kepteni wake wa zamani Roy Keane anasema: 'Ni mchezaji Staa anaeshangaza!! Hana makuu!!'
Nae Mfaransa Laurent Blanc aliekuwa Nahodha wa Ufaransa na aliewahi kuchezea Man U amesifia: 'Huwa namwambia kila mtu anaeniuliza- Scholes ndie bora Uingereza!!'
Sir Bobby Charlton, mwenyewe akiwa Mchezaji wa zamani alietukuka na kusifika, anatoa sifa za kipekee: 'Kuna Wachezaji niliowaabudu na wakapotea kwenye ajali ya ndege ya Timu ya Man U kule Munich, kuna Wachezaji kama Dennis Law na George Best ambao nilicheza nao, na sasa, kuna Wachezaji wa Sir Alex Ferguson ambao nawatizama lakini katika wote hakuna bora kama Paul Scholes!!'
Chelsea wabwaga manyanga!!! Wakiri kutwaa Ubingwa LIGI KUU ni ndoto!!
Meneja wa Chelsea, Guus Hiddink, baada ya Timu yake jana kutoka suluhu 0-0 na Everton na hivyo kujikuta wakiwa pointi 6 nyuma ya Man U ambao pia wana mechi moja mkononi huku Chelsea wakibakisha mechi 5 tu, amekiri Chelsea hawana matumaini tena ya kutwaa Ubingwa wa LIGI KUU.
Hiddink amekiri: 'Ingawa kimahesabu nafasi ipo lakini ukweli Man U wako mbali na ni bora tuwe wakweli na kukazania tu kwenye FA CUP ambako tuko Fainali na kwenye UEFA CHAMPIONS LEAGUE ambako tuko Nusu Fainali. LIGI KUU itabidi tutegemea wengine watusaidie ili tuwe Bingwa!! Hiyo haipo mikononi mwetu!!!'
Chelsea kwenye Fainali ya FA CUP itakayochezwa Mei 30 watakumbana na Everton. Kwenye Nusu Fainali UEFA CHAMPIONS LEAGUE wanachuana na Barcelona.
ROY KEANE AUKWAA UMENEJA IPSWICH TOWN!!
Nahodha wa zamani wa Manchester United, Roy Keane, ameteuliwa kuwa Meneja mpya wa Timu ya Ipswich Town ambayo inachezea Daraja la chini ya LIGI KUU England liitwalo Coca Cola Championship.
Keane alikuwa Meneja wa Timu ya LIGI KUU Sunderland hadi alipong'atuka mwenyewe mwezi Desemba 2008 baada ya kutoelewana na Bodi ya timu hiyo.
Keane aliteuliwa kuwa Meneja wa Sunderland Agosti 2006 wakati huo Sunderland ikiwa ipo nafasi ya pili toka mwisho kwenye Ligi ya Coca Cola Champioship na msimu huohuo akamudu kuipandisha daraja na kuiingiza LIGI KUU.

No comments:

Powered By Blogger