Wednesday 22 April 2009

Scholes kufikisha mechi ya 600 leo?

Paul Scholes [34,] endapo atapangwa katika Kikosi cha Manchester United kinachoshuka Old Trafford leo usiku kupambana na Portsmouth katika mechi muhimi sana ya LIGI KUUambayo Man U wanataka washinde ili wawe pointi 3 juu ya Liverpool, basi atafikisha mechi 600 katika Klabu yake tangu aanze kuichezea mwaka 1994.
Ni Wachezaji watatu tu waliochezea mechi nyingi Manchester United kumzidi Paul Scholes katika historia ya Klabu hiyo nao ni Ryan Giggs, mechi 798, Sir Bobby Charlton, mechi 758 na Bill Foulkes, mechi 658.
Meneja wake, Sir Alex Ferguson, anamsifia: 'Katika wakati wangu hapa Old Trafford, bila shaka yeye yupo katika listi ya Wachezaji 6 au 7 bora.'
Ni Mchezaji ambae hapendi makuu na ni mkimya sana. Kila awezapo, yeye huwakimbia Waandishi wa Habari.
Inasemekana aliwahi kusema anapenda kucheza soka lakini hapendi kuwa Mwanasoka
.


MECHI ZA LEO LIGI KUU England:
[saa 4 usiku bongo taimu]
Man U v Portsmouth
Chelsea v Everton

No comments:

Powered By Blogger