Saturday 25 April 2009

LIGI KUU England WIKIENDI HII: [Saa ni za Bongo]

JUMAMOSI, 25 April 2009
[Saa 11 jioni]
Bolton v Aston Villa
Everton v Man City
Fulham v Stoke
Hull v Liverpool
West Brom v Sunderland
West Ham v Chelsea
[Saa 1 na nusu usiku]

Man U v Tottenham


JUMAPILI, 26 April 2009
[Saa 9 na nusu]
Arsenal v Middlesbrough
[Saa 12 jioni]
Blackburn v Wigan


JUMATATU, 27 April 2009
[Saa 4 usiku]
Newcastle v Portsmouth

Man U: Wanashughulikia Tevez kubakia hapo!
Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, amesema wanashughulikia suala la Carlos Tevez kuendelea kubaki Klabuni hapo huku kukiwa na tetesi nyingi kuwa Mchezaji huyo huenda akaondoka mwishoni mwa msimu mkataba wake wa kucheza hapo kwa mkopo utakapoisha.
Ferguson ametamka: 'Tunaifanyia kazi ishu hiyo. Muhimu ni kuwa Tevez mwenyewe anapenda kubaki hapa.'
Fabregas na Phil Brown, Meneja wa Hull, matatani na FA!!
FA, Chama cha Soka England, kimewafungulia mashtaka Nahodha wa Arsenal, Cesc Fabregas, na Meneja wa Hull City, Phil Brown, kufuatia tafrani zilizotokea kwenye mechi kati ya Arsenal na Hull ya Kombe la FA ambyo ilichezwa katikati ya Machi na Arsenal kushinda 2-1.
Fabregas anakabiliwa na mashtaka mawili, moja likiwa ni vitendo vyake baada ya kuingia uwanjani mechi ilipomalizika na la pili ni kumtemea mate Meneja Msaidizi wa Hull, Brian Horton.
Siku hiyo Fabregas alikuwa si Mchezaji kwani alikuwa majeruhi.
Nae Phil Brown anakabiliwa na mashtaka ya kuuingiza mchezo kwenye kashfa kufuatia kauli zake baada ya mechi za kumkashifu Refa Mike Riley.
Watuhumiwa wote wawili wamepewa mpaka Mei 12 ili kujibu mashtaka hayo.

No comments:

Powered By Blogger