Sunday 19 April 2009

Ni Chelsea, Everton Fainali FA CUP!!!

Everton wamemudu kuingia Fainali ya FA CUP na sasa watakutana na Chelsea hapo Mei 30 baada ya kuwashinda Man U kwa penalti katika pambano lililoisha 0-0 na lililochezwa hadi muda wa nyongeza wa dakika 30 baada ya mechi kuwa sare. Ilikuwa mechi ambayo Sir Alex Ferguson aliwashangaza wengi kwa uteuzi wa timu 'chekechea' iliyokuwa na Wachezaji wengi wadogo na wa akiba na wawili tu ambao ndio 'vigogo', yaani Ferdinand na Vidic.
Hata hivyo, ingawa ilikuwa Man U 'hafifu', mechi ilkuwa nguvu sawa na pengine katika dakika 90 za kawaida hata Man U wangeweza kushinda kwa jinsi walivyopata nafasi na hata kunyimwa penalti ya dhahiri pale Welbeck alipoangushwa kwenye boksi.
Everton walishinda penalty 4-2 huku Cahill akikosa yao moja na waliofunga Man U ni Vidic na Anderson na wakosaji ni Berbatov na Ferdinand.
Man Utd:
Foster, Rafael Da Silva, Ferdinand, Vidic, Fabio Da Silva, Welbeck, Gibson, Anderson, Park, Tevez, Macheda.
Akiba: Kuszczak, Neville, Evra, Berbatov, Nani, Scholes, Evans.
Everton: Howard, Hibbert, Jagielka, Lescott, Baines, Osman, Neville, Fellaini, Pienaar, Cahill, Saha.
Akiba: Nash, Yobo, Castillo, Vaughan, Jacobsen, Rodwell, Gosling.
Refa: Mike Riley (Yorkshire)

MATOKEO LIGI KUU LEO:
Tottenham 1 Newcastle 0
Man City 4 West Brom 2

No comments:

Powered By Blogger