Sunday 25 May 2008







EURO 2008
JUNI 7-JUNI 29, 2008 nchini SWITZERLAND & AUSTRIA

Mashabiki wengi wa soka wanangojea kwa hamu Mashindano ya TIMU ZA TAIFA BARA LA ULAYA, EURO 2008, ambayo yatachezewa kwenye nchi mbili kwa pamoja, yaani USWISI na AUSTRIA, yatakayoanza 7 JUNI 2008 uwanjani ST JAKOB PARK, mjini BASLE, SWITZERLAND kwa mechi kati ya wenyeji wenza SWITZERLAND dhidi ya CZECH REPUBLIC.
Mechi ya FAINALI itachezwa Jumapili 29 JUNI 2008 uwanjani ERNST HAPPEL, VIENNA, AUSTRIA.
Timu za Mataifa 16 ya Ulaya zitashiriki zikigawanywa katika makundi manne ya timu 4 kila moja zitazocheza mechi za awali kwa njia ya ligi. Miongoni mwa timu hizo 16 ni wenyeji wenza AUSTRIA na SWITZERLAND.
MAKUNDI:
KUNDI A-CZECH, URENO, USWISI, UTURUKI

KUNDI B- AUSTRIA, CROATIA, UJERUMANI, POLAND,

KUNDI C- UFARANSA, ITALIA, UHOLANZI, ROMANIA

KUNDI D- UGIRIKI, URUSI, SPAIN, SWDEN

No comments:

Powered By Blogger