Sunday 25 May 2008


HULL CITY YATINGA LIGI KUU UINGEREZA!!!


HULL CITY 1 BRISTOL CITY 0


HULL CITY, kwa mara ya kwanza katika historia yao ya miaka 104, imefika kileleni mwa soka ya UINGEREZA baada ya kushinda fainali ya mtoano wa kuingia LIGI KUU UINGEREZA kwa kuifunga BRISTOL CITY 1-0 katika UWANJA WA WEMBLEY.

Kazi nzuri aliyoifanya chipukizi wa MAN U, FRAZIER CAMPBELL mwenye miaka 20, ambae yuko HULL CITY kwa mkopo, ilimfikia mkongwe DEAN WINDASS, mwenye miaka 39, ambae alifunga bao safi la ushindi. [PICHANI NI CAMPBELL AKIMRUKIA WINDASS KUSHANGILIA GOLI]


Timu hiyo ya HULL CITY ina maveterani wengine kama JAY JAY OKOCHA ambae hakucheza kwa kuwa ni majeruhi na NICK BARMBY ambae alicheza na kubadilishwa kipindi cha pili.


HULL CITY imeungana na WEST BROMWICH ALBION na STOKE CITY kuingia LIGI KUU UINGEREZA ambayo inatarajiwa kuanza msimu wa mwaka 2008/2009 mwezi AGOSTI.

No comments:

Powered By Blogger