Friday 30 May 2008


INTER MILAN WAMTIMUA MENEJA ROBERTO MANCINI!
inasemekana yuko njiani kuelekea STAMFORD BRIDGE--CHELSEA!!!!
Meneja wa Mabingwa wa Serie A, INTER MILAN, Roberto Mancini, amefukuzwa huku kukiwa na tetesi kubwa kuwa yuko njiani kujiunga na CHELSEA ambao siku tano zilopita walimtimua Meneja wao AVRAM GRANT.
Uvumi huu umezidi kujengewa imani baada ya Chelsea nao kumtimua kazi aliekuwa Meneja Msaidizi, Mholanzi HENK TEN CATE ambae alijiunga na CHELSEA mara tu baada ya kuteuliwa AVRAM GRANT kuwa Meneja wa klabu hiyo. Hatua hii ya Chelsea inaonekana na wadadisi wa mambo kama kumjengea njia meneja mpya aje na utawala wake mpya.

No comments:

Powered By Blogger