Monday 26 May 2008



MENEJA ALIETIMULIWA ASIFU UZOEFU ALIOUPATA CHELSEA!!!

Myahudi Avram Grant, aliemwaga unga CHELSEA, amerudi kwao Israel jana na kusema kuwa amepata uzoefu mkubwa alipokuwa klbuni hapo.

Pia akatoa shukrani za dhati kwa Wayahudi wenzake kwa jinsi walivyomuunga mkono alipokuwa akiiendesha Chelsea.
Nae Meneja aliemtangulia Avram Grant hapo Chelsea, Mreno Jose Mourinho amekanusha vikali kuwa kuna mipango ya yeye kurudishwa tena Chelsea.
Kuna habari pia msimu ujao Jose Mourinho atarudi tena kwenye viwanja ingawa si Chelsea.

No comments:

Powered By Blogger