Tuesday 27 May 2008


GERARD PIQUE ARUDI BARCELONA!


FC BARCELONA na MANCHESTER UNITED zimeafikiana uhamisho wa chipukizi GERARD PIQUE mwenye umri wa miaka 21 kurudi tena kwenye klabu yake aliyoihama 2004 ya BARCELONA.

Mlinzi huyo Mhispania alidumu MAN U kwa miaka 4 alianza mechi 14 na kuingizwa katika mechi 9 akitokea benchi la akiba. Aliifungia MAN U magoli mawili katka LIGI YA MABINGWA WA ULAYA msimu huu katika mechi dhidi ya DYNAMO KIEV na AS ROMA.

Inasemekana MAN U italipwa pauni za Kiingerezamilioni 6 [SHS BILIONI 14 ZA KIBONGO] kama ada ya uhamisho.

No comments:

Powered By Blogger