Thursday 29 May 2008


UINGEREZA 2 USA 0

Jumatano usiku katika Uwanja wa Wembley, Timu ya Taifa ya Uingereza iliifunga Timu ya Taifa ya Mrekani [USA] kwa mabao 2-0 kwenye mechi ya kirafiki.
Goli la kwanza lilifungwa na Nahodha John Terry kwa kichwa kufuatia cross murua ya David Beckham. Goli la pili lilipachikwa na Steven Gerrard.
Jumapili, timu hiyo ya Uingereza itakumbuna na Trinidad and Tobago katika mechi nyingine ya kirafiki.
*********************************************************************************
REAL MADRID WANYWEA!
Kisanga cha Cristiano Ronaldo kusakwa kwa udi na uvumba na Klabu ya Real Madrid kimechukua hatua mpya baada ya Klabu hiyo kunywea kufuatia Man U kutishia kuishitaki FIFA.
Rais wa Real, Ramon Calderon, amesema wao ni marafiki na Man U na hawataki kugombana nao.

No comments:

Powered By Blogger