Monday 26 May 2008


RONALDO: 'NINA FURAHA MAN U'
Nyota wa MAN U amesema ana mapenzi makubwa kuwa MANCHESTER UNITED ingawa angependelea siku moja acheze huko Spain.
Alisema: 'Magazeti siku zote yanaandika si REAL tu wananitaka hata BARCELONA pia. Ni vizuri kujua unazivutia klabu kubwa kwani hii inadhihirisha una thamani. Lakini kwa sasa kichwa changu kipo MAN U. Sasa, kama nilivyosema mara nyingi tu, ni Mungu pekee anaejua nini kitatokea hapo baadae. Sijamficha mtu kuwa ningependa hapo baadae kucheza Spain. Hiyo ni ndoto yangu lakini mara nyingi ndoto haziji. Nakuhakikishia nina mapenzi MAN U na ningependa kuendelea hapo.'

No comments:

Powered By Blogger