Sunday 31 August 2008

SASA REAL YAMEWAKUTA!!!!!!
ROBINHO ALIA: 'Niacheni nijiunge na Chelsea!'
Leo mbele ya Waandishi wa habari Mbrazil Robinho ambae ni mchezaji wa Real Madrid amekitangaza kilio chake na kudai aachiwe ajiunge Chelsea kabla ya kesho ambayo ni siku ya mwisho ya uhamisho wa wachezaji.
Robinho ambae ameonyesha kutofurahishwa na kubaki Real Madrid ameachwa kwenye kikosi cha timu hiyo kitakachocheza mechi ya kwanza ya msimu wa Primera Liga leo huko Spain zidi ya Deportivo la Coruna.
Robinho amedai kwamba tangu Mei alibembeleza mkataba wake uboreshwe lakini alipuuzwa kwa sababu Real walikuwa na uhakika wa kumsaini Cristiano Ronaldo.
Hata hivyo Robinho ameihakikishia Real kuwa endapo hatahama basi ataichezea klabu kwa moyo mmoja.

No comments:

Powered By Blogger