Monday 1 September 2008

PRIMERA LIGA:
VIGOGO REAL MADRID NA BARCELONA WAANZA LIGI KWA VIPIGO!!!!
Jana mechi za kwanza za ligi huko Spain ijulikanayo kama PRIMERA LIGA zilichezwa huku vigogo Barcelona na Real Madrid wakikung'utwa kwenye mechi hizo za kwanza.
Real Madrid walisafiri hadi nyumbani kwa Deportivo la Coruna bila ya nyota Robinho anaelilia kuhamia Chelsea na kupigwa mabao 2-1.
Nao Barcelona wakicheza nyumbani kwao walifungwa na timu iliyopanda daraja msimu huu Numancia kwa bao 1-0!
Nyota wa Barcelona Samuel Eto'o na Lionel Messi wote walipiga mashuti yaliyogonga mwamba!

No comments:

Powered By Blogger