Thursday 4 September 2008

UINGEREZA YAPOROMOKA KWENYE LISTI YA FIFA YA TIMU ZA TAIFA BORA!!!!!


-Tanzania iko nafasi ya 117!!!


Wakati nchi zikiwa zinaingia kwenye mitoano wikiendi hii ya kutafuta timu zitazocheza Fainali Kombe la Dunia huko bondeni Afrika Kusini mwaka 2010 Timu ya Taifa ya Spain ndiyo timu bora duniani kwa miezi mitatu mfululizo kufuatia listi iliyotolewa na FIFA.
Uingereza imeporomoka nafasi moja na kushika nafasi ya 15 ikiwa chini ya Cameroun ambayo ndio timu inayoshika nafasi ya juu kabisa kutoka Afrika ikiwa ipo nafasi ya 14 kwa ubora duniani.
Ghana pia iko kwenye ishirini bora ikishikilia nafasi ya 20.
Timu ya Taifa ya Tanzania iko nafasi ya 117 huku jirani zetu Rwanda, Kenya na Uganda wakiwa juu yetu wakifuatana kwa kushika nafasi ya 85 kwa Rwanda, 86 kwa Kenya na 87 kwa Uganda.
Katika Afrika timu iliyokuwa chini kabisa ni Jamhuri ya Afrika ya Kati ikiwa nafasi ya 199.
Timu ya mwisho kabisa duniani ni American Samoa ambayo iko nafasi ya 200 huku ikifungana na nchi nyingine kadhaa.
NAFASI 20 ZA JUU NI IFUATAVYWO [KWENYE MABANO NAFASI ZA AWALI]:
1. Spain (1), 2. Italy (3), 3. Germany (2), 4. Netherlands (4), 5. Croatia (5), 6. Brazil (6), 7. Argentina (7), 8. Czech Republic (8), 9. Portugal (9), 10. Turkey (13)11. France (12), 12. Russia (10), 13. Romania (11), 14. Cameroon (15), 15. England (14), 16. Scotland (16), 16. Bulgaria (17), 18. Greece (18), 19. Israel (20), 20. Ghana (19)

No comments:

Powered By Blogger