Wednesday 3 September 2008

MENEJA WA WEST HAM ALAN CURBISHLEY AACHIA NGAZI!
Alan Curbishley amekuwa Meneja wa kwanza wa klabu ya Ligi Kuu Uingereza kuachia ngazi wakati leo alipotangaza kujiuzulu kufuatia kutoridhika na mwenendo wa klabu kuuza wachezaji bila kumhusisha kikamilifu.
Siku chache zilizopita West Ham walimuuza mdogo wake Rio Ferdinand, mlinzi Anton Ferdinand kwa Klabu ya Sunderland na pia mchezaji mwingine George Mc Cartney bila ridhaa yake.
Wakati huohuo, Kevin Keagan, Meneja wa Newcastle yuko kwenye mvutano mkubwa na wamiliki wa klabu hiyo ambao walitaka kuwauza wachezaji bila ridhaa yake. Wachezaji wanaohusishwa na mfarakano huu, ingawa hawajauzwa, ni Michael Owen na Joey Burton.

No comments:

Powered By Blogger