Monday 1 September 2008

SIKU YA MWISHO UHAMISHO WACHEZAJI:
Pavlyuchenko na Corluka waingia Spurs!!!
Mshambuliaji Mrusi Roman Pavlyuchenko [26] na Mlinzi wa Croatia Vedran Corluka [22] wamesaini mikataba ya kujiunga na Tottenham Hotspurs leo ikiwa ndio siku ya mwisho ya kuhamisha Wachezaji.
Pavlyuchenko ni Mchezaji wa Timu ya Taifa ya Urusi iliyofana sana EURO 2008 na ametokea Klabu ya Spartak Moscow ya huko Urusi.
Nae Corluka ni Mchezaji wa Taifa wa Croatia na ameshaichezea Croatia mara 24. Klabu yake ilikuwa ni Manchester City aliyojiunga nayo mwaka 2007.


No comments:

Powered By Blogger