Sunday 26 April 2009

Arsenal 2 Middlesbrough 0

Wakati Arsenal, kwa ushindi wa leo, wanazidi kujichimbia kwenye nafasi ya 4 ya msimamo wa ligi na hivyo kupata nafasi ya kucheza UEFA CHAMPIONS LEAGUE msimu ujao, Middlesbrough wamezidi kuganda nafasi ya tatu toka chini na hivyo wako kwenye hatari kubwa kuporomoka daraja huku wakiwa wamesaliwa na mechi 4 tu.
Nahodha Fabregas ndie alifunga bao zote mbili za Arsenal na kuwafanya wafikishe pointi 65 wakiwa nafasi ya nne huku Chelsea wakiwa mbele yao wakiwa na pointi 71.
Middlesbrough wako nafasi ya 18, ikiwa ni ya tatu toka chini, na wana pointi 31 huku juu yao wapo Hull City pointi 34. Chini ya Middlesbrough wako Newcastle United pointi 30 na wa mwisho ni West Bromwich pointi 28.
Timu tatu za mwisho ndio huporomoshwa daraja
Arsenal: Almunia, Eboue, Toure, Silvestre, Gibbs, Walcott, Denilson, Fabregas, Nasri, Arshavin, Bendtner.
Akiba: Fabianski, Diaby, Sagna, Vela, Song Billong, Djourou, Adebayor. Middlesbrough: Jones, McMahon, Wheater, Huth, Taylor, O'Neil, Bates, Sanli, Downing, Aliadiere, King.
Akiba: Turnbull, Hoyte, Digard, Emnes, Alves, Adam Johnson, Grounds.
Refa: Chris Foy

Blackburn 2 Wigan 0

Jana, Benni McCarthy na Nahodha Nielsen waliifungia mabao Blackburn na kuifanya ijiwekee kizingiti cha pointi 6 na zile timu zilizo kwenye balaa la kushuka daraja.
Blackburn: Robinson, Ooijer, Nelsen, Givet, Warnock, Diouf, Grella, Kerimoglu, Pedersen, Samba, McCarthy.
Akiba: Bunn, Dunn, Khizanishvili, Andrews, Villanueva, Olsson, Doran.
Wigan: Kirkland, Boyce, Scharner, Bramble, Figueroa, Valencia, Watson, Cattermole, N'Zogbia, Mido, Rodallega.
Akiba: Pollitt, Edman, Koumas, De Ridder, Kapo, Zaki, Brown.
Refa: Peter Walton

No comments:

Powered By Blogger