Wednesday 29 April 2009

NDANI YA NOU CAMP: Barcelona 0 Chelsea 0
Barcelona wakiwa kwao Nou Camp huku kila mtu akitegemea Messi, Eto’o au Henry atafunga wameambua patupu baada ya Chelsea kufunga milango yote.
Barcelona: Valdes, Dani Alves, Marquez (Puyol 52), Pique, Abidal, Xavi, Toure Yaya, Iniesta, Messi, Eto'o (Bojan 82), Henry (Hleb 87).Akiba hawakucheza: Jorquera, Gudjohnsen, Keita, Sylvinho.
Kadi: Toure Yaya, Puyol.
Chelsea: Cech, Ivanovic, Alex, Terry, Bosingwa, Mikel, Ballack (Anelka 90), Essien, Lampard (Belletti 71), Malouda, Drogba.Akuba hawakucheza: Hilario, Di Santo, Kalou, Mancienne, Stoch.
Kadi: Alex, Ballack.
Watazamaji: 95,000.
Refa: Wolfgang Stark (Germany).
REFA WEBB akiri kosa!!
Refa Howard Webb aliechezesha mechi ya Manchester United na Tottenham uwanjani Old Trafford na Man U kuibuka washindi 5-2 wakati walikuwa nyuma 2-0 hadi hafutaimu amekubali alikosea kuipa Man U penalti kipindi cha pili na ambayo Ronaldo aliifungia timu yake bao la kwanza.
Webb amesema: ‘Nimeangalia tena na nadhani ni kosa lakini sisi huwa tunatoa uamuzi wa haki pale pale. Sisi tuko uwanjani na nilimwona Mchezaji wa Manchester akiucheza mpira na kuangushwa lakini sikuona Kipa akiugusa mpira ule. Inasikitisha lakini nionyeshe mtu asiefanya makosa na mimi ntakuonyesha mtu asiefanya chochote!’
Penalti hiyo imezua mzozo mkubwa hadi Kiungo wa Tottenham Jermaine Jenas ametakiwa na FA ajieleze ndani ya siku 7 kwa kauli yake ya kumkashifu Refa.
Lakini wadau wengi wanajiuliza hata kama Refa alikosea na 'KUIBEBA' Man U kupata bao la kwanza walikuwa wapi mabao mengine 'HALALI' 'MANNE; kuingia?
Hakika mfa maji haishi kutapatapa!!!!!

No comments:

Powered By Blogger