Saturday 2 May 2009

LEO NI 'EL CLASICO': Real Madrid v Barcelona!!!

Kwa wapenzi wa La Liga, yaani Ligi ya Spain, leo kivumbi kitatimka ndani ya Uwanja wa Santiago Bernabue, nyumbani kwa Real Madrid watakapo wakaribisha watani zao Barcelona.
Kukiwa kumebaki mechi 5 ligi kumalizika, Barcelona wanaongoza kwa pointi 4 huku Real Madrid wakiwanyemelea.
Barcelona wamekuwa wakiongoza ligi hiyo karibu msimu mzima na katika mechi 33 wamefunga mabao 94 lakini Real Madrid tangu wafungwe na Barcelona 2-0 Desemba huko Nou Camp uwanjani kwa Barcelona hawajapoteza mechi yeyote.
Mechi hii itaanza saa 3 usiku saa za bongo.

No comments:

Powered By Blogger