Monday 9 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

O'Neill atimka Villa
Martin O'Neill amejiuzulu kama Meneja wa bila kutaja sababu za zilizomfanya achukue uamuzi huo.
O’Neill alianza kazi hapo Aston Villa Mwaka2006 na kuifanya Klabi hiyo iwe ikimaliza Ligi Kuu katika nafasi za juu na Msimu uliokwisha ilishika nafasi ya 6 hiyo ikiwa ni kwa mara ya tatu mfululizo.
Kevin MacDonald ameteuliwa kuwa Meneja wa muda.
NGAO YA HISANI: Man United 3 Chelsea 1
• Man United yaonyesha kuwa tishio Msimu mpya!
Manchester United hapo jana iliifumua Chelsea kwa bao 3-1 na kutwaa Ngao ya Hisani katika pambano lililochezwa Uwanja wa Wembley Jijini London.
Mbele ya Mashabiki 84,623 waliokuwa wakiwazomea Wachezaji wa England waliocheza Kombe la Dunia huko Afrika Kusini, Kiungo mkongwe wa Manchester United, Paul Scholes aling’ara na kuibuka kuwa Mchezaji Bora wa Mechi hiyo.
Man United walipata bao la kwanza kwa Soka tamu kati ya Scholes na Rooney na mpira kupelekewa Valencia aliefunga.
Mchezaji mpya wa Man United, Javier Hernandez, maarufu kama Chicharito, alionyesha cheche zake na kuamsha matumaini makubwa kwa Washabiki wa Man United na ndie aliefunga bao la pili.
Chelsea walipata bao lao kupitia Salomon Kalou baada ya Kipa Edwin van der Sar kutema shuti la Daniel Sturridge.
Vikosi:
Chelsea: Hilario, Paulo Ferreira (Bruma 79), Ivanovic, Terry, Cole (Zhirkov 79), Essien, Lampard, Mikel (Drogba 60), Kalou, Anelka (Sturridge 60), Malouda (Benayoun 72).
Akiba hawakucheza: Turnbull, Van Aanholt.
Man Utd: Van der Sar, O'Shea, Jonathan Evans, Vidic, Fabio Da Silva (Smalling 71), Valencia, Scholes (Fletcher 80), Carrick (Giggs 79), Park (Nani 46), Owen (Hernandez 46), Rooney (Berbatov 46).
Akiba hawakucheza: Kuszczak.
Refa: Andre Marriner

No comments:

Powered By Blogger