Tuesday 5 October 2010

TEMBELEA TOVUTI YENYE SURA MPYAAAAA: www.sokainbongo.com

Tevez afarakana na Mancini
Straika wa Manchester City Carlos Tevez aligombana na Meneja wake Roberto Mancini wakati wa mapumziko wa mechi ya Ligi Kuu Jumapili ambayo Man City waliifunga Newcastle 2-1.
Inadaiwa mzozo kati yao ulianza pale Tevez, Nahodha wa Timu hiyo, alipotukana kwa lugha ya Kispanish na Mancini kusikia ndipo wakaanza kurushiana maneno.
Inasemekana Tevez alikuwa ameudhiwa na mbinu za Mancini za kulundika Wachezaji wengi kwenye Kiungo na kumuacha yeye kama Straika pekee na hivyo kukosa mipira ya kufunga.
Hii ni mara ya pili kwa Tevez na Mancini kukwaruzana mara ya kwanza ilikuwa pale Tevez aliponukuliwa na Magazeti akiponda jinsi Mancini anavyoendesha mazoezi ya Timu.
Mancini amekuwa hana uhusiano mzuri na baadhi ya Wachezaji na tayari alishakwaruzana na Craig Bellamy na kumfanya Mchezaji huyo apelekwe Cardiff City kwa mkopo.
Pia ameshagombana na Emmanuel Adebayor ambaye amekuwa hapewi namba.
Torres nje Wiki kadhaa
Fernando Torres atakuwa nje ya uwanja kwa wiki kadhaa akiuguza musuli za kwenye nyonga na hiyo imemfanya asiitwe kwenye Kikosi cha Spain kitakachocheza mechi za EURO 2012 wiki hii na ijayo dhidi ya Lithuania na Scotland.
Torres, Miaka 26, alicheza dakika 10 tu za mechi ya Ligi Kuu Jumapili iliyopita ambayo Liverpool ilichapwa 2-1 Uwanjani kwao Anfield na Blackpool.
Pia kuumia huko kutamfanya Torres aikose dabi ya Liverpool na Watani zao Everton itakayochezwa Oktoba 17 huko Goodison Park.
Tangu Msimu uliokwisha Torres amekuwa akiandamwa na majeruhi ya mara kwa mara.
Spain yataja Kikosi cha mechi za EURO 2012
Kocha wa Spain, Vicente del Bosque, ametangaza Kikosi cha Spain kitakachocheza mechi za EURO 2012 hapo Oktoba 8 na Lithuania na Oktoba 12 na Scotland huku Mastaa kama Fernanbdo Torres wa Liverpool, Fowadi wa Barcelona Pedro na Winga wa Sevilla Jesus Navas, wakiachwa baada ya kuumia.
Badala yake Kocha del Bosque amelazimika kuchukua Wachezaji wapya, wawili kutoka Valencia, Aritz Aduriz na Pablo Hernandez, na wawili kutoka Villareal, Borja Valero na Bruno Siriano.
Kikosi kamili:
Makipa: Iker Casillas (Real Madrid), Victor Valdes (Barcelona), Pepe Reina (Liverpool)
Mabeki : Alvaro Arbeloa (Real Madrid), Sergio Ramos (Real Madrid), Carles Puyol (Barcelona), Gerard Pique (Barcelona), Carlos Marchena (Villarreal), Joan Capdevila (Villarreal), Nacho Monreal (Osasuna)
Viungo : Xabi Alonso (Real Madrid), Sergio Busquets (Barcelona), Santi Cazorla (Villarreal), Andres Iniesta (Barcelona), Pablo Hernandez (Valencia), Borja Valero (Villarreal), Bruno Soriano (Villarreal)
Mafowadi : David Villa (Barcelona), David Silva (Manchester City), Fernando Llorente (Athletic Bilbao), Aritz Aduriz (Valencia)
KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA
RATIBA:
Ijumaa, 8 Oktoba 2010
Libya v Zambia
Mali v Liberia
Senega lv Mauritius
Zimbabwe v Cape Verde
Namibia v Mauritania
Central African Republic v Algeria
Togo v Tunisia
Comoros v Mozambique
Jumamosi, 9 Oktoba 2010
Malawi v Chad
Kenya v Uganda
Tanzania v Morocco
Burundi v Ivory Coast
Rwanda v Benin
Cameroon v Congo DR
Angola v Guinea-Bissau
Burkina Faso v Gambia
Jumapili, 10 Oktoba 2010
Sierra Leone v South Africa
Ghana v Sudan
Madagascar v Ethiopia
Niger v Egypt
Congo v Swaziland
Guinea v Nigeria

No comments:

Powered By Blogger