Thursday 4 March 2010

England 3 Misri 1
Mabingwa wa Afrika, Misri, waliianza mechi hii ya kirafiki Uwanjani Wembley, kwa kuwashtukiza England na kupachika bao dakika ya 23 mfungaji akiwa Zidan, bao ambalo lilidumu hadi mapumziko.
Kipindi cha pili England walizinduka na kufunga bao 3, wafungaji wakiwa Peter Crouch, mabao mawili dakika ya 56 na 80, na Shaun Wright-Phillips, dakika ya 75.
Katika mechi hii kikundi kidogo cha Mashabiki kilikuwa kikimzomea Nahodha wa zamani wa England, John Tery, alievuliwa cheo hicho kwa kashfa, lakini baadae walikuwa wakimshangilia.
Kwa England, kufuatia kuumia kwa Ashley Cole na kugoma kucheza kwa Wayne Bridge, Beki ya kushoto ilizibwa na Leighton Baines wa Everton ambae alicheza vizuri na huenda akaikwaa namba hiyo kwa kudumu.
Kwa ujumla, Mabingwa wa Afrika, Misri, walicheza vizuri na hawakustahili kufungwa bao la 3 la Crouch kwani mfungaji alikuwa ofsaidi.
VIKOSI:
England: Green, Brown, Terry, Upson, Baines, Walcott (Wright-Phillips 57), Lampard (Carrick 46), Barry, Gerrard (Milner 73), Rooney (Cole 86), Defoe (Crouch 46).
Akiba hawakucheza: James, Warnock, Lescott, Shawcross, Beckham, Heskey, Downing, Hart.
Egypt: El Hadari, Al-Muhammadi, Said (Salem 86), Fathi, Gomaa, Ghaly, Moawad (Abdelshafy 76), Hassan (Nagy 64), Abd Rabou, Zidan (Aboutreika 76), Ebdelmaby (Zaki 64).
Akiba hawakucheza: El Sayed, Fathallah, Tawfik, El Saka, Raouf, Eid, Hamdy.
MATOKEO: Mechi za Kirafiki za Kimataifa
Jumanne, Machi 2
Ireland 0 v Brazil 2
Jumatano, Machi 3
Albania 1 v Northern Ireland 0
Algeria 0 v Serbia 3
Angola 1 v Latvia 1
Austria 2 v Denmark 1
Belgium 0 v Croatia 1
England 3 v Egypt 1
France 0 v Spain 2
Germany 0 v Argentina 1
Greece 0 v Senegal 2
Hungary 1 v Russia 1
Italy 0 v Cameroun 0
Ivory Coast 0 v South Korea 2
Nerthelands 2 v USA 1
Portugal 2 v China 0
Poland 2 v Bulgaria 0
Scotland 1 v Czech Republic 0
Slovakia 0 v Norway 1
Slovenia 4 v Qatar 1
South Africa 1 v Namibia 1
Switzerland 1 v Uruguay 3
Turkey 2 v Honduras 0
Wales 0 v Sweden 1

No comments:

Powered By Blogger