Wednesday 13 August 2008

KIMBEMBE KWA ARSENAL NA LIVERPOOL LEO!!
-FC TWENTE vs ARSENAL
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amekiri kuwa leo watu wengi wanategemea Arsenal wataifunga FC Twente katika mechi ya Raundi ya Tatu ya LIGI KLABU ULAYA inayochezwa Uholanzi na hivyo kuzidisha presha kwa Arsenal.
FC Twente inafundishwa na Steve McClaren aliekuwa Meneja wa Timu ya Taifa ya Uingereza kazi aliyotimuliwa Novemba 2007.
Arsenal imeenda Uholanzi bila mastaa wao kadhaa ambao ni majeruhi. Waliomo kwenye listi hiyo ni Fabregas, Kolo Toure, Abou Diaby, Tomas Rosicky, Philippe Senderos, Eduardo na Mchezaji mpya Samri Nasri.
Mechi hii itachezwa saa 3 dakika 45 usiku kwa saa za bongo. Mechi ya marudiano ni tarehe 27 Agosti kwenye Uwanja wa Emirates.
-STANDARD LIEGE vs LIVERPOOL
Liverpool leo saa 4 dakika 5 usiku huu watakuwa nchini Ubelgiji kupambana na Mabingwa wa Ubelgiji Klabu ya Standard Lige kwenye mechi ya Raundi ya Tatu ya LIGI KLABU ULAYA.
Liverpool imeshuka huko na kikosi chao kamili isipokuwa mchezaji Steve Finnan ambae inasemekana amegombana na Meneja wake Rafael Benitez.
Timu itachaguliwa kutokana wachezaji wafuatao:Reina, Arbeloa, Carragher, Agger, Dossena, Kuyt, Gerrard, Alonso, Benayoun, Torres, Keane.Subs (from): Cavalieri, Plessis, Ngog, Spearing, Hyypia, Pennant, Darby

No comments:

Powered By Blogger