Monday 11 August 2008

KLABU BINGWA ULAYA
MCHUJO WAPAMBA MOTO!!!!!!!!!!!!

Mechi za Raundi ya Tatu ya Mtoano katika mashindano ya LIGI YA KLABU BINGWA ULAYA zinachezwa Jumatano tarehe 13 Agosti na marudiano ni Agosti 27.
Timu zilizoshika nafasi ya tatu na ya nne katika LIGI KUU UINGEREZA, Arsenal na Liverpool, zimo kwenye raundi hii.
Arsenal imepangwa kukutana na timu ya Uholanzi FC Twente inayoongozwa na aliekuwa Meneja wa Timu ya Taifa ya Uingereza Steve McClaren ambae alitimuliwa kazi hiyo Novemba 2007. Liverpool itakutana na Standard Liege ya Ubelgiji.
Arsenal na Liverpool wataanza mechi zao ugenini.
Washindi 16 wa mechi hizi watajumuika na timu nyingine 16 ambazo ni Mabingwa wa Nchi na washindi wa pili wa ligi za nchi [Timu kutoka Uingereza ni Mabingwa Man U na washindi wa pili Chelsea] kufanya jumla ya timu 32 zitakazogawanywa makundi manane ya timu 4 kila moja zitakazocheza mtindo wa ligi.
Mechi hizi za makundi zitaanza tarehe 16 Septemba na kumalizika Desemba 10.

RATIBA KAMILI: [TIMU INAYOTAJWA KWANZA NDIO MWENYEJI]
Anorthosis v Olympiakos

Vitoria Guimaraes v Basel

Shakhtar v Dinamo Zagreb

Schalke 04 v Atletico Madrid

Aalborg v Kaunas

Barcelona v Wisla Krakow

Levski Sofia v Bate

Standard Liege v LIVERPOOL

Partizan v Fenerbahce

FC Twente v ARSENAL

Spartak Moscow v Dinamo Kiev

Juventus v Artmedia

SK Brann v Marseille

Fiorentina v Slavia Prague

Galatasaray v Steaua Bucharest

Sparta Prague v Panathinaikos

No comments:

Powered By Blogger