Monday 11 August 2008

Portsmouth wamchukua Kaboul toka Spurs
Portsmouth wamefanikiwa kumsaini Mlinzi Younes Kaboul kutoka Tottenham.
Mfaransa huyu amesaini mkataba wa miaka minne baada ya vuta ni kuvute na Klabu za Sunderland na Aston Villa ambazo pia zilikuwa zinamgombea.
Kaboul, 22, alijiunga Tottenham Hotspurs kwa Pauni milioni 8 kutoka Klabu ya Ufaransa Auxerre mwezi July mwaka jana lakini alichezeshwa mechi 18 tu na Tottenham.

West Brom wamsaini Meite kutoka Bolton
West Bromwich Albion wamemnunua mchezaji wa Ivory Coast Mlinzi wa kati Abdoulaye Meite kutoka Bolton Wanderers kwa Pauni milioni 2.
Abdoulaye Meite mwenye umri wa miaka 27 ambae pia anaweza kucheza kama beki wa pembeni amesaini mkataba wa miaka mitatu kwa ada ya Pauni milioni 2 na nusu.
Meite alijiunga na Bolton mwezi Julai 2006 baada ya kuichezea Marseille ya Ufaransa kwa miaka mitano.
Alicheza mechi 56 alipokuwa na Bolton.

No comments:

Powered By Blogger