Sunday 10 August 2008


NGAO YA HISANI

MAN U 0 PORTSMOUTH 0
MAN U washinda kwa penalty 3-1!!
Mabingwa wa Ulaya na Uingereza wamefunua rasmi pazia la msimu wa 2008/9 kwa kuutawala kabisa mchezo uliochezwa nusu uwanja kwa muda mrefu dhidi ya Mabingwa wa Kombe la FA Portsmouth ingawa walishindwa kupata goli katika dakika 90.
Nafasi za wazi zilikoswa na MAN U na Refa alichangia baada ya kuwanyima penalti ya wazi pale Carlos Tevez aliposhikwa mguu na Mlinzi Hreidarsson ndani ya boksi.
Baada ya dakika 90 ikaja tombola ya penalti:
-MAN U wakafunga kupitia Tevez, Giggs na Carrick
-Portsmouth walikosa ya kwanza aliyopiga Diarra, kisha Defoe akafunga, Mvuemba na Johnson wakakosa zilizofuata.
VIKOSI VILIKUWA:
Man Utd: Van der Sar, Neville (Brown 66), Ferdinand, Vidic, Evra, Fletcher, O'Shea (Carrick 66), Scholes, Giggs, Nani (Campbell 79), Tevez. AKIBA HAWAKUCHEZA: Kuszczak, Evans, Possebon, Da Silva.
Portsmouth: James, Johnson, Campbell, Distin, Hreidarsson (Lauren 79), Diop, Pedro Mendes (Mvuemba 75), Diarra, Kranjcar (Utaka 60), Crouch, Defoe. AKIBA HAWAKUCHEZA: Ashdown, Sahar, Cranie, Traore.
WATAZAMAJI: 84,808

No comments:

Powered By Blogger