Sunday 10 August 2008

KAMPUNI YA RIO KUFYATUA ALBAMU YA KWANZA!!!

Staa wa MANCHESTER United Rio Ferdinand akitumia kampuni yake iliyoko Manchester iitwayo Chalk Records watafyatua albamu yao ya kwanza huku yeye binafsi akishirikishwa kidogo kwenye treki ya kwanza ya albamu hiyo.
Mfokaji wa kike aitwae Nia Jai ndie msanii wa albamu hiyo iitwayo ‘Black Ice’ itakayosambazwa Oktoba 1.
Kampuni ya Chalk Records iliianzishwa miaka miwili iliyopita na Rio Ferdinand akaanzisha shindano maalum kumtafuta msanii ataetoa albamu ya kwanza na kampuni yake.
Nia Jai, mwenye umri wa miaka 25 ambae ni muuguzi kitaaluma, alishinda shindano hilo na anammwagia sifa kubwa Rio Ferdinand kwa msaada aliompa hadi kufikia hatua ya kukaribia kuiingiza sokoni albamu hiyo.
Rio anamsifia msanii huyo kuwa ana bidii na kipaji maalum.

No comments:

Powered By Blogger