Saturday 9 August 2008


PAZIA LA MSIMU 2008/9 KUFUNGULIWA KESHO!

MAN U vs PORTSMOUTH

kugombea NGAO YA HISANI

Uwanja wa Wembley mjini London, Uingereza kesho Jumapili saa 11 jioni saa za bongo utakuwa unafungua pazia la msimu wa Soka wa 2008/9 wa Uingereza kwa pambano kati ya Mabingwa wa LIGI KUU Manchester United na Mabingwa wa Kombe la FA Portsmouth watakapogombea NGAO YA HISANI.
Manchester United ndio Mabingwa watetezi wa Ngao hiyo baada ya kuwashinda Chelsea mwaka jana kwa penalti.
Portsmouth mara ya mwisho kulishika kombe la aina hii ni mwaka 1949 walipotoka suluhu na Wolverhampton na ikabidi wagawane kombe hilo kwa miezi sita sita.
Timu hizi mbili zilikutana mara ya mwisho mjini Abuja, Nigeria wiki mbili zilizokwisha katika mechi ya kirafiki ambayo Man U walishinda 2-1.
Timu zote zina majeruhi kadhaa na watakao kuwa nje kwa Man U ni Ronaldo, Rooney, Park, Hargreaves na Saha. Man U inategemewa itawachezeshaji chipukizi kutoka Brazil ambao wako timu yao ya akiba ambao ni ndugu mapacha Fabio na Rafael Da Silva pamoja na Possebon.
Portsmouth huenda ikakawakosa Kanu, Lauren na Nugent.
Refa katika mechi hii atakuwa Peter Walton ambae ameteuliwa dakika za mwisho tu baada ya Refa aliepangwa Mark Clattenburg kusimamishwa na FA na PGMO [Uongozi wa Marefa wa Kulipwa] kutokana na Kampuni zake kufilisika.
Wachezaji wanategemwa kuwa:
Manchester United : Van der Sar, Kuszczak, Neville, Brown, R Da Silva, Ferdinand, Vidic, O'Shea, Evans, Evra, Silvestre, F Da Silva, Nani, Carrick, Scholes, Fletcher, Gibson, Possebon, Giggs, Martin, Tevez, Campbell.
Portsmouth : James, Johnson, Campbell, Distin, Hreidarsson, Utaka, Diop, Pedro Mendes, Kranjcar, Crouch, Little, Sahar, Diarra, Defoe, Davis, Kanu, Wilson, Duffy, Lauren, Nugent, Mvuemba, Cranie, Ashdown.

No comments:

Powered By Blogger