Sunday 3 August 2008




Ferguson kumpa nafasi chipukizi Frazier Campbell
Meneja wa MAN U, Sir Alex Ferguson, amesema chipukizi Frazier Campbell atapewa nafasi kucheza kwenye kikosi cha kwanza cha MAN U kwa sababu ana uwezo wa kufunga, mwepesi, mpiganaji mzuri na amethibitisha hayo baada ya kung’ara katika ziara ya Afrika ya hivi karibuni.
Frazier Campbell, miaka 20, jana alifunga goli la ushindi katika mechi ya kumuaga nyota wa MAN U, Ole Gunnar Solskjaer, hapo jana dhidi ya Espanyol ya Spain. MAN U ilishinda 1-0.

Vilevile, chipukizi huyu alikuwa mmoja wa wachezaji walioisaidia sana Hull City kupanda daraja na kuingia LIGI KUU UINGEREZA wakati alipoichezea timu hiyo kwa mkopo msimu ulopita.
Ferguson alitamka: ‘Ni mwepesi na ana bidii sana. Hapo baadae atakuwa nyota hapa. Tunategemea kupata kibali cha Manucho [Mchezaji mshambuliaji toka Angola] atasaidia kuimarisha safu ya washambuliaji. Campbell na Manucho ni muhimu kwani tuna upungufu safu hii. Tuna Washambuliaji wawili tu- Rooney na Tevez.’

No comments:

Powered By Blogger