Friday 8 August 2008

Jens Lehmann astaafu kuchezea Ujerumani
Kipa Jens Lehmann [umri miaka 38] ametangaza kustaafu kuchezea Timu ya Taifa ya Ujerumani.
Kipa huyo wa zamani wa Arsenal ametoa uamuzi huo mara baada ya mkutano na Meneja wa Ujerumani Joachim Low.
Lehmann ameichezea Ujerumani mara 61 katika kipindi cha miaka 10 na mara ya mwisho ilikuwa kwenye Fainali ya EURO 2008 walipofungwa na Spain ambayo ilitwaa ubingwa huo.
Lehmann alijiunga na Arsenal mwaka 2003 na juzi tu amehamia Klabu ya Stuttgart ya Ujerumani kwa mkataba wa mwaka mmoja.

Wengi wanategemea atastaafu soka baada ya mkataba huu kumalizika.

No comments:

Powered By Blogger